Tangazo

Pages

Tuesday, May 1, 2012

MABONDIA WAWILI WA TANZANIA WATINGA ROBO FAINALI


                                                                                                                                         Tuesday, May 01, 2012
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:

 YAH:- MABONDIA WAWILI WATANZANIA WATINGA HATUA YA ROBO KATIKA MASHINDANO YA KUFUZU     
                          KUELEKEA OLIMPIKI YANAYOENDELEA CASSABLANCA MOROCCO.
Mobondia wa  timu ya taifa waTanzania Selemani Kidunda  69 kgs welter weight na Emillian Patrick      56 kgs bantam weight wamesonga mbele katika mashindano ya kufuzu kuelekea katika kushiriki mashindano ya Olimpiki yatakayofanyika London Uingereza,katika mashindano yaliyoanza tarehe 28/4-5/5/2012 Casablanca Morocco.
Mabondia hao wamefika hatua hiyo baada ya kushinda mapambano yao ya awali kwa seleman Kidunda kumshinda Kab Thiam wa Senegal kwa RSC na Emillian Patrick kumshinda Tewodros Tilahun wa Ethiopia.
Mabondia hao sasa wamefika katika hatua ya robo fainali ambapo ni jumla wa mabondia nane waliofikia hatua hiyo na idadi inayotakiwa kufuzu ni mabondia sita kwa kila uzito.
Mabondia hao kesho tarehe 2/5/2012 watapanda ulingoni kwa Emillian Patrick kucheza na Isaac Dogboe  wa Ghana  na Seleman Kidunda atacheza na Mehdi Khalsi wa Morocco .
Endapo watashinda watakuwa wameingia hatua ya nusu fainali na tayari watakuwa wamefikia hatua ya kupata medali ya shaba .
Tanzania ilipeleka jumla ya wachezaji wanne na viongozi wawili wachezaji wawili Victor Njaiti na Abdalah Kassim walitolewa katika hatua za awali.                                                                                                      viongozi walioambatana na timu ni Michael Changarawe na Remmy Ngabo.
Aidha kesho kutafanyika mkutano mkuu wa Shirikisho la ngumi la Afrika (AFBC) Tanzania katika mkutano huo itawakilishwa na makamo wa Rais wa BFT Michael Changarawe
Kwa niaba ya BFT tunawaomba watanzania wote kila mmoja kwa imani yake kuwaombea ili washinde na wafuzu  kushiriki mashindano ya Olimpiki kwa kuzingatia kuwa kwa upande wa ngumi tulishiriki olimpiki kwa mara ya mwisho mwaka 1996 Atlanta.
Makore Mashaga
Katibu Mkuu (BFT)        0713 588818.

No comments:

Post a Comment