Tangazo

Pages

Thursday, July 30, 2020

MABONDIA ABDALLA PAZI NA TWAHA KIDUKU WATAMBULISHA MPAMBANO WAO WA AUGUST 28 UWANJA WA UHURU

Mabondia Abdallah Pazi kushoto na Twaha Kiduku wakiangaliana kwa usongo wakati wa kutambulisha mpambano wao utakaofanyika katika uwanja wa Uhuru August 28 katikati ni Promota wa mpambano uho Jay Msangi 'Jiwe Gumu'

Promota wa mpambano wa masumbwi nchini Jay Msangi 'Jiwe Gumu' katikati akiwatambulisha mabondia Abdallah Pazi kushoto na Twaha Kiduku watakaopambana August 28 katika uwanja wa Uhuru Dar esa Salaam

SUPER D AMNOWA JUMA CHOKI KUJIANDAA KUMKABILI EMANUEL MWAKYEMBE AUGUST 14 MLIMAN CITY


Bondia Juma Choki kushoto askioneshana Umwamba wa kutupiana makonde na bondia wa kimataifa Ibrahimu Class wakati wa mazoezi yake katika Kambi ya Super D Coach Shule ya Uhuru ya kujiandaa na mpambano wake na Emanuel Mwakyembe utakaofanyika Augost 14 Mlimani City Dar Es Salaam



Bondia Vicent Mbilinyi kushoto akipambana na Juma Choki katika mazoezi yaliyofanyika katika Kambi ya Super  D Coach Shule ya Uhuru Dar Esa salaam Choki anajiandaa na mpambano wake na Emanuel Mwakyembe utakaofanyika augost 14 katika ukumbi wa Mlimani City
Na Mwandishi Wetu

Bondia Juma Choki anaye jiandaa na mbambano wake dhidi ya Emanuel Mwakyembe AUgust 14 katika ukumbi waMlimani City jijini Dar es es salaam amejinasibu kumpiga bondia huyo na kuendeleza ubabe baada ya mara ya kwanza kumpiga na kuwa bingwa wa ubingwa wa king of The Ring katika mashindano yaliyofanyika mwaka jana

akijinasibu bondia huyo alivyotembelewa kambini kwake kwa Super D Coach iliyopo shule ya Uhuru Jijini Dar es salaam 

Amesema kuwa mwakembe ana uwezo wa kukanyaga moto wake ata siku moja kwani kichapo alichompa mara ya kwanza kitakuwa zaidi ya kile 
naomba mashabiki waje kuangalia kichapo nitakachompa ulingoni 
 kwani ndipo pa kuoneshana uwezo kama anavyosemaga kocha Super D Kazi Kazi No Pain No Gain yani siku hiyo patachimbika hivyo mwakyembe ajipange sana kwana mazoezi ninayofanya na mbinu ninazofundishwa sio za kitoto hatari tupu

Nae kocha wa bondia huyo Rajabu Mhamila 'Super D' amesema hii ni vita kubwa sana kwa kuwa kocha wa mwakyembe  Edward Lwiyakwipya wamesoma nae pamoja katika ngazi kubwa ya kozi ya kimataifa hata hivyo mimi nina mbinu nyingi zaidi yake ndio mana nilimtwanga katika mpambano wa kwanza na sasa naenda kupiga begi langu tena ata hivyo nita akikisha napata ushindi usiokuwa wa kuwachosha majaji hivyo matumaini yangu ni kumpiga k,o mbaya zaidi

ikumbukwe kuwa mabondia wote wenye viwango vya juu nchini wanatoka kwangu ukiangalia mabondia wote wakubwa wanatoka kwangu
wanakuwa na viwango vya kimataifa hivyo najivunia kwa hilo ukiangalia mabondia wanaotoka kwangu akuna ata mchovyu mmoja alijinasibu Super D

Aliongeza kwa kusema mikono yake wamepita mabondia wengi sana akiwemo Sanday Kiwale, Idd Mkwera Vicent Mbilinyi Ibrahimu Class' King Class Mawe' Shomali Milundi  Shabani Kaoneka na mabondia mbalimbali nchini wote wamepita katika mikono yangu kwa njia moja au nyingine hapa ndio No Pain No Gain kazi kazi hivyo wapenzi wa ngumi muje kwa wingi kuangalia kazi hii ambayo aita muacha mtu salam siku hiyo katika viwanja vyua mlimani City

Thursday, July 9, 2020

BONDIA HASSANI MWAKINYO ATANGAZA MPAMBANO WAKE WA AGOST 14 MLIMANI CITY ATAMVAA TSHIBANGU KAYEMBE WA DRC YA CONGO

Bondia Hassani Mwakinyo kushoto akizungumza na wahandishi wa habari wakati akitangaza mpambano wake wa Agost 14 utakaofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Dar Esa Salaam Tanzania wa pili ni Mlatibu wa mpambano uho Beatrice Said na kulia ni bondia Tonny Rashidi nae atamsindikiza Mwakinyo siku hiyo Picha na Super D


Mlatibu mkuu wa mapambano Beatrice Said kulia ambaye ameandaa mchezo wa masumbwi yatakayofanyika Agost 14 akiwa na bondia Tonny Rashidi atakae tetea ubingwa wake huo na Gabriel Ochieng wa Kenya  

Mratibu wa mpambano wa masumbwi Beatrice Said akiwa na bondia Hassani Makinyo wakati wa kutangaza mpambano wake wa agost 14 utakaofanyika katika ukumbi wa mlimani city




BONDIA Mtanzania Hassan Mwakinyo anatarajia kupanda ulingoni Agosti 14 mwaka huu kumenyana na Bondia kutoka DRC ya Congo Tshibangu Kayembe.
Pambano hilo la aina yake la kuwania ubingwa wa WBF linatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Mlimani city ambapo mabondia hao watapambana raundi 12.
Akizungunzia mtanange huo Mwakinyo amesema yuko tayari kwa pambano hilo kwani amejiandaa vya kutosha kuhakikisha anamaliza pambano hilo mapema.
Amesema, maandalizi mazuri ambayo ameyafanya na kuendelea kuyafanya yanazidi kumpa morali zaidi kuelekea pambano hilo ambalo hatokubali kuiangusha Nchi.
"Tarehe 14 mwezi ujao natamani sana pambano lifike hata siku zikimbie ziwe tano tano, nimejiandaa na naendelea kujiandaa sina shaka wala hofu na bondia yoyote yule aje tu tukutane ulingoni,"
Aidha Mwakinyo alimuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuri kuunga mkono jitihada za mabondia hapa nchini kama ambavyo amefanya mambo makubwa katika kuendeleza  nchi na jina lake kuzidi kuwa kubwa.
Anasema Rais akisapoti mchezo huo hata wao mabondia itakuwa vyema kwao na itazidi kuwapa morali ya hali ya juu kuzidi kulitangaza Taifa.
"Naimani kubwa na Rais wetu pia nawaomba wadhamini nao wasiutupe mchezo wetu huu unapeperusha vyema bendera ya Tanzania kupitia sisi na hiyo Agosti 14 nitawahahakikishia Watanzania mimi ni nani,"
Kwa upande wake Mratibu wa matukio kuelekea pambano hilo Beautrice Said amesema katika pambano hilo kutakuwa na mapambano ya utangulizi nane ya utangulizi ambayo yatawakitanisha mabondia wa hapa Tanzania.
Baadhi ya mapambano hayo ni Seleman Kidunda ambaye ataumana na Shaban Kaoneka uzito kg 72, Issa Nampepecha na Khareed Manjee kg 61.
Pia katika pambano hilo kutakuwa na pambano lingine la Kimataifa ambalo litamkutanisha Tony Rashid atakayemualika Mkenya Gabriel Ochieng pambano la raundi 12 kutetea ubingwa wa ABU.
Mwakinyo amepambana mapambano 18 na kupoteza mawili huku mpinzani wake Kayembe amecheza mapambano 12 kashinda 9 na kutoka sare 3. 

aliongeza kwa kusema kuwa mapambano mengine yatawakutania bondia Juma Choki dhidi ya Emanuel Mwakyembe na Baina Mazola atamkabili Haidari Mchanjo mbali na mapambano hayo kutakuwa na mapambano kumi kabla ya mpambano mkubwa wa Mwakinyo