Tangazo

Pages

Friday, September 30, 2016

MABONDIA KUPIMA UZITO KESHO JUMAMOSI KWA AJILI YA MPAMBANO WAO WA OCTOBER 2 KIMARA KOROGWE

Na Mwandishi Wetu

BABONDIA mbalimbali watakaozipiga siku ya jumapili ya October 2 katika ukumbi wa White House Bar Kimara Korogwe watapima uzito pamoja na Afya zao kesho jumamosi katika ukumbi uho kwa ajili ya kuzipiga siku inayo fuata

akizungumzia mpambano uho kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini ambaye ni mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa mabondia wote watapia uzito pamoja na Faya Zao siku ya jumamosi

aliwataja baadhi ya mabondia watakaozipiga na kesho watapima uzito ni Said Chino atakaezitwanga na haidar Mchanjo uzito wa kg 57 raundi sita wakati Abdallah Ruwanje atavaana na Shedrack Ignas mpambano wa raundi sita la uzito wa kg 63wakati bondia mkongwe kabisa katika mchezo wa masumbwi nchini Mustafa Doto atazipiga na bondia chipkizi Manyi Issa katika uzito wa kg 61 raundi sita

mipambano mingine itawakutanisha mabondia Mohamed Muhunzi atakaepambana na Kassim Ahmad na Hashimu Chisora atazipiga na Rojas Masam uzito wa kg 61 na Julias Jackson atapambana na Emilio Norfat mpambano wa raund 4 uzito wa kg 61  na Ellsame Mbwambo atazipiga na Emanuel Kisawani mpambano wa raundi 4 uzito wa kg 61

siku hiyo pia kutakuwa na elimu ya ujasiliamali kwa vijana wa mchezo wa masumbwi pamoja na kupatiwa mafunzo mbalimbali ya kujikwamuwa na uchumi 

Mgeni rasmi katika mpambano uho atakuwa 
Humphrey Polepole Mkuu wa Wilaya ya Ubungo
 
Katika Mchezo huo kutakua na Uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha  'Super D' kwa ajili ya kuwapa mabondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi. 

Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi

MABONDIA DEO SAMWELI NA FABIAN LYMO WASAINI KUZIPIGA NOVEMBA MOSI MANZESE

Mabondia Deo Samweli kushoto na Fabian Lymo wakitunishiana misuli mbele ya promota wao Hassan Magole baada ya kuwasainisha mpambano wa raundi kumi utakaofanyika Novemba mosi katika ukumbi wa kobelo Pub Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS
Mabondia Fabian Lymo kushoto na Deo Samweli 
  wakitunishiana misuli 
baada ya kusainisha mpambano wa raundi kumi utakaofanyika Novemba mosi katika ukumbi wa kobelo Pub Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS

Rais wa Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBC Chaurembo Palasa kulia akishudia bondia Deo Samweli akitia saini kuzipiga na Fabian Lymo novemba mosi kushoto ni  promota wao Hassan Magole
Rais wa Kamisheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBC Chaurembo Palasa kulia akishudia bondia Fabian Lymo akitia saini kuzipiga na Deo Samweli novemba mosi kushoto ni  promota wao Hassan Magole




Mabondia Deo Samweli kushoto na Fabian Lymo wakitunishiana misuli mbele ya promota wao Hassan Magole baada ya kuwasainisha mpambano wa raundi kumi utakaofanyika Novemba mosi katika ukumbi wa kobelo Pub Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS

Mabondia Deo Samweli kushoto na Fabian Lymo wakitunishiana misuli mbele ya promota wao Hassan Magole baada ya kuwasainisha mpambano wa raundi kumi utakaofanyika Novemba mosi katika ukumbi wa kobelo Pub Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS


Thursday, September 22, 2016

MABONDIA KUZIPIGA OCTOBER 2 KIMARA KOROGWE NA KUPEWA ELIMU YA UJASILIAMALI


Na Mwandishi Wetu

ZAIDI ya Mabondia alobaini kupata elimu ya ujasiliamali katika mpaqmbano wa october 2 utakaofanyika katika ukumbi wa White House Bar uliopo Kimara Korogwe mbali na semina hiyo ya ujasiliamali na uwekezaji katika mchezo wa masumbwi pia wanamichezo hawo wata oneshana umwamba siku hiyo baada ya kupewa semina ya masaa mawili yanayo husu ujasiliamali

Akizungumza na wahandishi wa habari mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila 'Super D' amesema mpambano uho utakuwa zaidi ya mchezo mana kutakuwa na elimu mbalimbali zitakazo tolewa kwa vijana mbalimbali na watu watakao hudhulia siku hiyo

Elimu hiyo kwanza itatolewa October Mosi katika ukumbi huo huo utkao husisha makocha mabondia pamoja na wasaidizi wao mbalimbali watakaokuja siku moja kupima uzito na afya kabla ya mpambano wao sdiku inayo fuata mana vijana watafundishwa elimu ambayo itaweza kuwakwamua kimaisha pindi watakapo staafu mchezo wa ngumi

aliongeza kwa kusema mapambanop yatakayopigwa siku hiyo ni kati ya Abdallah Luwanje atakaezipiga na Shedrack Ignas uzito wa kg 63 raundi sita na haidar Mchanjo atazidunda na Said Chino katika uzito wa kg 57 raundi sitawakati bondia Mustafa Doto ataoneshana umwamba na Manyi Issa katika mpambano wa KG 61 raundi sita 

Wakati

Rojas Masamu

ataoneshana undava na Hashimu Chisora katika uzito wa kg 61 raundi nne na Mohamed Muhunzi atapambana na Kassim Ahamad katika uzito wa KG 56 raundi nne na mapambano mengine mengi yatakayokuwepo siku hiyo
Ambaya mgeni rasmi atakuwa 
Humphrey Polepole Mkuu wa Wilaya ya Ubungo
 
Katika Mchezo huo kutakua na Uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha  'Super D' kwa ajili ya kuwapa mabondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi. 

Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi

Thursday, September 15, 2016

JIFUNZE MASUMBWI NA SUPER D COACH

(ULINGO)
Buster amduwaza Mike Tyson
DVD ZA SUPER D BOXING COACH ZILIZOPO SOKONIFEBRUARI 11 mwaka 1990 jijini Tokyo nchini Japan, Mike Tyson alipoteza pambano lake la kwanza kwa Buster Douglas, ingawa alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kushinda.
Lakini kikubwa ambacho wengi hawakijui ni kwamba, Douglas alipanda ulingoni katika pambano hilo ikiwa ni siku 23 tu baada ya kumpoteza mama yake mzazi.
Mama yake Douglas, Lula Pearl alifariki siku 23 kabla ya pambano hilo baada ya kupatwa na ugonjwa wa kiharusi.
Hali hiyo mashabiki wengi waliichukulia kwamba ingempotezea kujiamini Douglas katika pambano na hivyo walikuwa na imani kubwa ya kulipoteza.
Wakati pambano hili linaanza, kambi ya Tyson ilikuwa ikishangilia kwa nguvu huku ikiamini kwamba atashinda kwa urahisi, hasa ikizingatiwa kwamba alikuwa hajawahi kupigwa tangu aanze masumbwi ya kulipwa ya uzito wa juu.
Tyson alifanikiwa kumpeleka chini Douglas katika raundi ya nane na hapo ndipo wengi waliamini mwisho wake umefika, lakini alihesabiwa na kufanikiwa kusimama.
Douglas alinyanyuka akiwa na nguvu ya ajabu, kwani katika raundi ya 10 alifanikiwa kusukumizia makonde mazito Tyson na kumpeleka chini ya sakafu.
Kudondoka kwa Tyson katika raundi hiyo, ndiyo ilikuwa ni mara yake ya kwanza katika kipindi chake cha uchezaji wa ndondi.
Mwamuzi wa pambano hilo Octavio Meyran alimhesabia mara 10 Tyson, lakini alishindwa kusimama na hivyo Douglas akatangazwa bingwa mpya.
Hata hivyo, kambi ya Tyson ilimlalamikia mwamuzi huyo kwamba alimhesabia kwa haraka, wakati kwa Douglas hakufanya hivyo wakati amedondoka.
Wengi waliamini kwamba Tyson aliathirika kisaikolojia kwa kushindwa kuamini kama amedondoshwa na hivyo kujikuta akiwa hana uwezo wa kusimama haraka.
Kipigo hicho cha Tyson ndiyo kinachukuliwa kuwa cha kushitukiza zaidi katika historia ya mchezo wa masumbwi duniani.
Aidha kipigo hicho cha Tyson kilikuja wakati ambao akishikilia mikanda mikubwa mitatu ya uzito wa juu duniani ambayo ni WBC, WBA na IBF.
Lakini kubwa zaidi ni kwamba Tyson alikuwa akipanda ulingoni katika pambano hilo akiwa na mahusiano mabaya na Robin Givens kiasi kilichochangia kutokuwa na maelewao mazuri na Meneja wake wa muda mrefu, Bill Cayton pamoja na promota wake Don King.
Pia Tyson alikuwa anatoka kumtema mkufunzi wake wa mazoezi wa muda mrefu, Kevin Rooney.
Tyson alipanda ulingoni kwenye pambano hilo akitoka kumchapa Carl William kwa KO kwa sekunde 93.
Na pambano hilo la Douglas lilichukuliwa kama ni la kujipima nguvu kabla ya kumvaa Evander Holyfield ambaye alijipambanua kutaka kupanda naye ulingoni.

MABONDIA MANYI ISSA NA MUSTAFA DOTTO KUONESHANA UMWAMBA OTCOBER 2 KIMARA

Mabondia Manyi Issa kushoto akitunishiana misuli na Mustafa Dotto baada ya kusaini mkataba kwa ajili ya kuzipiga Mustafa Dotto October 2 katika ukumbi wa white house kimara koroge Picha na SUPER D BOXING NEWS
Mabondia Manyi Issa kushoto akitunishiana misuli na Mustafa Dotto baada ya kusaini mkataba kwa ajili ya kuzipiga Mustafa Dotto October 2 katika ukumbi wa white house kimara koroge Picha na SUPER D BOXING NEWS
MUSTAFA DOTTO
Na Mwandishi Wetu

MABONDIA MBALIMBALI KUZIPIGA October 2 katika ukumbi wa White House Kimara Korogwe mabondia hawo ni Manyi Issa atakaezipiga na bondia mkongwe na mzoefu Mustafa Dotto katika uzito wa kg 61 na mpambano mwingine utawakutanisha maasimu Shedrack Ignas atakae zipiga na Abdalla Ruwanje  katika uzito wa kg 63 mpambano wa raundi sita

Mapambano hayo yameratibiwa na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'

aliongeza kwa kusema kuwa siku hiyo kutakuwa na mapambano mbalimbali ya masumbwi yatakayo kuwepo siku hiyo

mapambano mengine yatawakutanisha mabondia Emanuel Kisawani atakaezipiga na Ellsame Mbwambo katika uzito wa kg 61 wakati bondia Mohamed Muhunzi atapambana na Kassim Ahmad mpambano wa raundi nne KG 56 bondia machachali anaekuja juu zaidi katika mchezo wa masumbwi nchini Saidi Chino atazipiga na Haidali Mchanjo mpambano unao subiliwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa mchezo uhu wa masumbwi na ndio pambano litakalo beba michezo yote ya siku hiyo
Mabondia wengine watakao zichapa siku hiyo ni Athumani Yanga atakae oneshana ubabe na Hashimu Chisora katika uzito wa KG 61 wakati Karim Migea atavaana na Bright Nazad katika uzito wa kilo gram 61 na mpambano mwingine utawakutanisha Julias Jackson atakae vaana na Emilio Norfat mpambano wa raundi sita

Katika Mchezo huo kutakua na Uuzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha  'Super D' kwa ajili ya kuwapa mabondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi. 


Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi

JIFUNZE MASUMBWI NA SUPER D COACH

ULINGO
 
Pambano la Alfa na  Sorkitti ilikuwa balaa
 
HILI lilikuwa ni pambano kali kati ya  Muhammad Alfaridzi akijulikana maarufu kwa jina la ‘ Alfa’ lilikuwa dhidi ya Kongthawat Sorkitti aliyejulikana kwa jina la Thongchai Treeviset.
 
 Lilikuwa ni pambano kali lililofanyika Machi 30, 2004 ambapo Muhammad Alfaridzi, alisimamishwa katika raundi ya 8 kwa  KO. Kumbuka Alfaridzi aliyezaliwa Agosti 2, 1976 alikuwa anatimiza mika 25 wakati mpinzani wake wakati huo alikuwa na miaka 30.
 
Pambano
 
Lilikuwa ni pambano kali na la mchakamchaka, lakini ‘siku ya mwisho’ Kongthawat Sorkitti akaibuka na ushindi baada ya kumsimamisha Alfaridzi kwa ‘Knockout’ (KO) ya raundi ya nane na kutwaa ubingwa wa super featherweight.
 
 Raundi ya kwanza:
 
Kongthawat Sorkitti anaanza taratibu raundi huku Alfaridzi akionekana kukamia zaidi na kusukuma masumbwi kutaka kumaliza pambano mapema. ‘Jab’ za Alfaridzi zinatembea na zinamkamata Sorkitti, kwa muda mwingi Alfaridzi anatawala pambano na raundi ya kwanza inamalizika Alfaridzi akiongoza kwa pointi.
 
 Raundi ya pili na tatu:
 
Raundi ya pili  na tatu haikuwa tofauti na ya kwanza, katika raundi hizi mbili, Alfaridzi anaendelea kumshambulia Sorkitti kwa kutumia ‘jabs’ na ngumi mchanganyiko na Sorkitt anatumia muda mwingi kujihami na kurusha ngumi moja moja lakini kwa umakini mkubwa, raundi ya tatu kama zilivyo za pili na kwanza zinamalizika na Alfaridzi anakwenda kwenye kona akiwa na anaongoza kwa pointi.
 
 Raundi ya nne:
 
Raundi ya nne inabadilika, Sorkitti anaibuka na kuanza kusukuma makonde mazito, Alfaridzi anajaribu kumpunguza kasi lakini inakuwa si rahisi,  uzoefu unaonekana kumbeba zaidi Sorkitti, anatupa makonde ya uhakika zaidi na yanamkamata vizuri Alfaridzi na raundi inapomalizika Sorkitti anaongoza kwa pointi.
 
  Raundi ya tano na sita
  Raundi ya tano, Sorkitti anaendelea kusukuma makonde mazito kwa  Alfaridzi. Alfaridzi anapiga jab zake na ngumi zake za kulia ‘right’, lakini Sorkitti hampi nafasi, anambana Alfaridzi na kumpa kibano cha uhakika.
 
Raundi ya sita, kama ilivyokuwa raundi ya tano, Sorkitti anasukuma makonde mazito kwa Alfaridzi anayejikinga asiendelee kunyeshewa mvua za ngumi, Sorkitti anaonekana kupata nguvu zaidi na kuzidi kumpelekesha  Alfaridzi na sasa akipigana kwa nia ya ushindi zaidi, anapiga ngumi nzito na zinatua kichwani kwa Alfaridzi, raundi inamalizika Sorkiti anaongoza kwa pointi.
 
  Raundi ya saba:
 
Katika raundi hii, Alfaridzi anazidiwa dhahiri, anapokea makonde ambayo yanamzidi ‘umri’, Sorkitti anapiga ngumi ya kushoto inamkamata Alfaridzi, anapiga ya kulia inamkamata pia Alfaridzi, anayeyumba huku na kule na kusimama lakini kwa ‘mawenge’ akiendelea kukomaa lakini Sorkitti anasukuma ‘jab- jab’  kisha ‘right’ na kengele inalia kumaliza raundi hiyo na Sorkitti akiongoza tena raundi hiyo.
 
Raundi ya nane:
 
Sorkitti anaanza kwa nguvu zaidi na kumsukumia makonde Alfaridzi akitumia jab na ngumi mchanganyiko ‘combination’, anapiga ngumi ya kushoto ‘left’ kisha anaachia ngumi mkunjo kali ya kulia ‘rigt hok’ na inatua kwenye taya la Alfaridzi na anakwenda chini kama gunia la nyanya.
 
 Mwamuzi anamuhesabia, lakini inapofika sita, Alfaridzi haoneshi dalili za kusimama, timu yake kwenye kona inakimbilia ulingoni na kwa haraka wanamvua viatu na glavu na kuanza kumpepea wakimpa huduma ya kwanza bila mafanikio kwani Alfaridzi amepoteza fahamu kutokana na kipigo kile.
 
 Haraka Alfaridzi anakimbizwa hospitali ambako anafanyiwa upasuaji wa kichwa  na kuondolewa damu  iliyovia kwenye ubongo, lakini anabaki akiwa hana fahamu na akipumulia mashine kwa muda wa siku tatu na kisha kufariki dunia Aprili 2, 2004 akiwa na miaka 25.
 
 Kuna tetesi hata sasa kwamba bondia  Alfaridzi kabla ya pambano hilo alifanya fujo mtaani na watoto wa kihuni wakamtwanga fimbo kichwani. Siku chache baadaye akapanda ulingoni, hivyo kifo chake inasadikika kilianza na kupigwa kwake fimbo kichwani kwani huenda kulisababisha ufa kwenye fuvu la kichwa ambao uliongezewa na ngumi za Khongtawat Sorkitti siku ya pambano, kwani Alfaridzi hakuwahi kupima kichwa baada ya kupigwa fimbo ile mtaani.
 **Mwandishi ni kocha wa mchezo wa ngumi anayefundisha klabu mbalimbali Dar es Salaam. Anapatikana kwa simu 0713/0787- 406938 au email: superdboxingcoach@gmail.com

BONDIA IDDI MKWELA ASAINI KUZIPIGA NA ISSA NAMPEPECHE OCTOBER 23 MWANANYAMALA

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mghamila 'Super D' kushoto akisaini mkataba wa bondia Iddi Mkwela wa pili kushoto ambaye atazipiga october 23 na Issa Nampepecha kulia katika ukumbi wa CCM mwijuma Mwananamala katikati ni Ibrahimu Kamwe 'Bigryth' ambaye ni mlatibu wa mpambano uho Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Iddi Mkwela kushoto akitambiana na Issa Nampepeche mara baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Octobe 23 katika ukumbi wa CCM MWIJUMA Mwananyamala Picha na SUPER D BOXING NEWS

Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akiwa na mabondia Iddi Mkwela wa Pili kushoto Issa Nampepeche pamoja na Ibrahimu Kamwe mabondia hao wamesaini kuzipiga october 23 katika ukumbi wa CCM Mwijuma Mwananyamala Picha na SUPER D BOXING NEWS


BONDIA IDDI MKWELA AKISAINI MKATABA
ISSA NAMPEPECHE AKISAINI MKATABA
Bondia Iddi Mkwela kushoto akitambiana na Issa Nampepeche mara baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Octobe 23 katika ukumbi wa CCM MWIJUMA Mwananyamala Picha na SUPER D BOXING NEWS


Na Mwandishi Wetu

BONDIA IDDI Mkwela amesaini mkataba wa kuzipiga na Issa Nampepecha mpambano wa raundi kumi siku ya October 23 katika ukumbi wa CCM Mwijuma mpambambano wa raundi kumi uzito wa KG 61

Mpambano uho ulio ratibiwa na Ibrahimu Kamwe utawakutanisha mabondia vijana ambao ni wadogo sana katika mchezo wa masumbwi nchini na watazipiga raundi kumi siku hiyo

pia kutakuwepo na mapambano mbalimbali ya utangulizi siku hiyo

akiongea wakati wa utiaji saini mkataba uho bondia Mkwela amesema amejipanga vizuri kumpiga Nampepeche kwani atojali kuwa na bifu na watu mbalimbali ili mradi aeze kuibuka na ushindi wa nguvu siku hiyo

nae Nampepeche amesema kuwa anaendelea na mazoezi kama kawaida ivyo mashabiki wake wategemee ushindi tu kwani siku hiyo atakuwa uwanja wa nyumbani na atokuwa na msalia mtume

Katika Mchezo huo kutakua na Uuzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha  'Super D' kwa ajili ya kuwapa mabondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi. 


Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi