Tangazo

Pages

Friday, October 26, 2012

BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' APANIA KUWA BINGWA WA TAIFA



NI dhahiri kuwa vipaji vikiibuliwa tangu utotoni na kuendelezwa vyema vijana wanakuja kuwa wazuri ukubwani na kulitangaza vyema taifa nchi za nje.
Hali hiyo inadhihirika kwa kijana Ibrahim Class 'king Class Mawe' ambaye anafanya vizuri katika medani za ngumi  ambazo zinamsaidia kuinua kiwango chake.
Tangu aingie katika mchezo huo ameshiriki katika mashindano mengi na kufanya vizuri na kusababisha wadau mbalimbali wa masumbwi kumtabilia kufika mbali mbali ikiwa atazingatia mazoezi.
King Class anasema alishawishika kuingia katika mchezo huo kutokana na mapenzi aliyokuwa nayo tangu utotoni ambapo alikuwa na ndoto za kuwa mwanamasumbwi.
Anasema kuwa ndoto yake ilianza kutimia baada ya kaka yake naye anaeitwa Chaku Master kuwa mwanamasumbwi alikuwa akifanya vyema miaka kadhaa iliyopita.
Chaku nilikuwa nikiishin naye hivyo wakati anakwenda kufanya mazoezi nilimuomba kuongozana na hali iliyonifanya kuanza kucheza licha ya kuwa ni ndoto yangu ya siku nyingi, anasema King  Class.
Kocha wake wa kwanza kufundisha kucheza ngumi alikuwa ni mzee Babu Tule ambaye alimpa misingi ambayo inamfanya hadi kuwa bondia mzuri anaeshimu nidhamu na sheria za mchezo huo.
Mwaka mmoja baada ya kuwa na kocha huyo alimuamishia kwa kocha Mkongwa  Habibu Kinyogoli ambapo hapo alikutana na makocha wengi akiwemo kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'  ili kumpa mbinu zaidi za mchezo huo na kumjenga katika misingi thabiti ya kufikia ndoto za kifikia mafanikio.
Anasema mwaka 2006 baada ya kuwa chini ya kocha wa siku nyingi katika mchezo huo Kinyogoli kiwango chake kinakuwa kikiongezeka kila siku na kuwa tishio katika ngumi za amacha.
Class anasema tangu wakati huo amepambana mapambano mengi ambao alifanya vizuri na kumbukumbu yake inaonesha alifanikiwa kuwatwanga wapinzani kwa KO katika mapambano zaidi ya 10, ndicho kitu anachojivunia kwa sasa.
"Huwa najisikia faraja ninampompiga mtu kwa KO kwani inazidi  kunijengea heshima katika ngazi ya amacha ambayo ndiyo niliyopo kwa sasa ambayo nahisi sina mpinzani," anasema Class.
Anasema siri kubwa ya kufanikiwa kufanya vizuri katika mapambano yake ni kutokana na kuzingatia mazoezi, miiko, sheria na kanuni za mchezo huo ambazo kila siku huwa anaelekezwa na kocha wa Kinyogoli.
Chipkizi huyo katika masumbwi anasema kila bondia anaweza  kufanya vizuri ikiwa atajihidi kusimama imara kuzingatia yanayokatazwa katika mchezo huo.
"Moja ya vitu ambavyo avitakiwi ni uvutaji wa sigara na utumiaji wa dawa kulevya ikiwemo Bangi na dawa nyingine ambazo ufanya kuwa na uhamuzi usio sahihi," anasema Class.
Class anasema ikiwa bondia atatumia Sigara au akivuta bangi ufanisi wake unakuwa mdogo kutokana na kifua kuwa kizito na kushindwa kumaliza raundi za mchezo au anaweza kupigwa kwa KO.
Hivyo anawashauri mabondia ambao wanajihusisha utumiaji wa tumbaku kuhachana na tabia hiyo ili kufikia malengo waliojiwekea katika masumbwi.
Pia anasema unywaji wa pombe nayo ni sehemu inayonyong'onyesha viungo, ikiwa bondia atahitaji kufanya vizuri ni vyema akaepiuka utumiaji wa pombe.
Kingine anasema kuwa suala la uzinzi nalo ni tatizo kwa baadhi ya wanasumbwi na ndiyo sababu kubwa inayowafanya kushindwa kufanya vyema ulingoni na kuambulia kupigo kikali.
Hivyo anawaomba wanamasumbwi chipukizi na wakongwe kujiepusha na hanasa hizo ambayo zinarudisha nyuma harakati za maendeleo ya mchezo huo nchini.
Kijana huyo aliyemaliza  taehe 10/10/1990 na kupata elimu yake ya msingi katika Shule ya  msingi Mafinga mwaka 2000, mkoani Iringa anasema  licha ya kujihusisha na masumbwi pia ni fundi wa vifaa vya umeme ikiwemo pasi, TV, Friji,specer na vifaa vyote vinavyotumia umeme.

Anasema ili kuundeleza mchezo  ni bora vifaa vikatolewa kwenye klabu mbalimbali zinazoinua mchezo huu kwa vijana wadogo ambao mara wamekuwa wakitatizwa na nyenzo za kufanyia mazoezi.
King Class Mawe kwa sasa aliemia katika ngumi za kulipwa na kufanya vizuri katika mapambano yake ya awali ikiwemo kumtwaga bondia Sako Mwaisege kwa K,O ya raundi ya tatu na kufanikiwa kumdunda bondia mkongwe wa mchezo huo Jonas Segu kwa point na kufanikiwa kuweka rekodi yake ya masumbwi kuwa nzuri

Bondia huyo kwa sasa yupo kambini kwa ajili ya mpambano wake na bondia kutoka Tanga Said Mundi utakaofanyika Desemba 9 katika ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar es salaam


King Class Mawe kwa sasa yupo chini ya kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' kwa ajili ya kuakikisha kipaji chake kinakuwa na anapata michezo mbalimbali hapa nchini na matarajio yake ni kuwa bingwa wa Taifa na bingwa wa Dunia kupitia mchezo wa Masumbwi



--

Rajabu Mhamila 'Super D'
Photojournalist at Majira, Business Times
           mhamila1@gmail.com


        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

No comments:

Post a Comment