Tangazo

Pages

Sunday, October 7, 2012

TPBO YAMSISITIZIA KAIKE SIRAJU KUWALIPA MABONDIA



Na Elizabeth John
OGANIZESHENI ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO) imesema kama promota wa ngumi nchini, Siraju Kaike (Pichanihatowalipa mabondia chipukizi, watalazimika kumfungia leseni yake kwa muda au mwaka mzima.
Kaike anadaiwa kuwafanyia kitendo ambacho si cha kiungwana mabondia chipukizi Issa Omar na Mwaite Juma kwa kuwapambanisha Julai 15 mwaka huu kwa makubaliano ya kuwalipa na baadae kutowalipa.
Juni 25 mwaka huu Kaike aliwasainisha mkataba mbele ya Katibu Mkuu wa Ngumi za Kulipwa Tanzania , Ibrahim Kamwe, kuwa Omar kucheza na Ramadhan Kumbele kwa malipo ya sh. 80,000.
Akizungumza Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa TPBO, Ibrahim Kamwe alisema uongozi wa oganizesheni hiyo wamekuwa wakimsihi kila siku awalipe mabondia hao na kukubali, lakini
mabondia wakienda kwake anawapiga kalenda.
Alisema kitendo hicho si cha kiungwana hivyo wamewashauri mabondia hao waende mahakamani ili waweze kupata haki yao na kuwapa nguvu wao ya kumsimamishia eseni yake kwa muda ili awe na adabu.
“Hatuna haja ya sisi tuseme kwamba tunamfungia, ukizingatia kiasi chenyewe ni kidogo na Kaike ana uwezo wa kulipa, nashangaa kwa nini anasubiri mpaka aambiwe wakati ni jukumu lake kuwalipa mabondia, anabaki kuwapiga kalenda tu, mara njoeni kesho mara kesho kutwa” alisema Kamwe.
Alipotafutwa Kaike kwa kupitia simu yake ya mkononi, ilikuwa inaita bila kupokelewa na baadae ikazimwa kabisa.

No comments:

Post a Comment