Tangazo

Pages

Wednesday, October 10, 2012

AMIR KHAN: NIKIDUNDWA TENA NITAFIKIRIA UPYA



LONDON, England
BONDIA Amir Khan aliyepoteza makali katika mapambano yake ya karibuni na kuamua kumtimua kazi mkufunzi wake, amesisitiza kutorejea tena makosa yatakayomnyima ushindi ulingoni wakati atakapomvaa Carlos Molina.
Bingwa huyo wa zamani wa dunia uzani wa ‘light-welterweight,’ anhaha kulizika jinamizi la kuvurunda lililomfanya apoteze mapambano yake mawili ya mwisho alipoangukia pua dhidi ya Lamont Peterson na kisha Danny Garcia.
Na sasa Khan anatambua fika kuwa kukubali kichapo cha tatu mfululizo atakapopambana na Molina hapo Desemba 15 jijini Los Angeles, Marekani, sio tu kutaporomosha heshima yake ulingoni, bali pia kutampotezea matumaini ya kuzichapa na Ricky Hatton.
Tangu alipochapika kwa KO dhidi ya Garcia, Khan alijikuta akipoteza heshima yake ulingoni, kabla ya kuamua kuachana na mkufunzi wake Freddie Roach na kumpa kazi Virgil Hunter – aliyemuita kocha bora duniani katika kumpa bondia uwezo wa kujilinda ulingoni.
Khan, 25, alifichua: “Sitaki kamwe kupoteza pambano hili. Sitaki tena kuwa katika nafasi hiyo ya kupoteza pambano tena, kama nitapoteza, basi nitafikiria, ‘Wapi napoweza kwenda kufanya kitu baada ya hapa?’
“Presha yangu ya mchezo iko juu kushinda pambano hili. Ni kufa au kupona. Hilolimenifanya nibadilike kwa asilimia 100 katika kila idara, kila kitu kiko kwenye mstari. Nataka kuhakikisha sifanyi tena makosa ulingoni.”
Hatton anarejea rasmi ulingoni baada ya kutoonekana huko kwa miaka mitatu tangu Novemba 24 alipopanda ulingoni MEN Arena katika mji wa kuzaliwa wa Manchester na tayari amejinasibu kuhakikisha anamtandika Khan Desemba 15.

No comments:

Post a Comment