Tangazo

Pages

Saturday, April 25, 2015

CORETION ZA DVD ZA MAYWEATHER NA PACQUAIO SASA ZINAPATIKANA UHURU / MSIMBAZI DAR


Na Mwandishi Wetu 

IKIWA zimesalia siku chache kufanyika mpambano wa kusisimua wa mchezo wa masumbwi Duniani kati ya bondia Floyd Mayweather na Manny Paquaio mei 2 mwaka uhu mpambano uho uliovunja rekodi ya mapato mbalimbali ya ngumi zilizofanyika kwa kipindi hichi

kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amekwisha toa Coretion  DVD  za mapambano ya wakali hawo yaliyopita nyuma dvd hizo zenye mafunzo mbalimbali pamoja na mazoezi wakati wakijiandaa kupigana mpambano wao

ambao utafanyika mei 2 Super D alisema nimetoa video zao ili watu wazione pamoja na kumbukumbu zao za nyuma ambapo kila DVD moja ina mapambano manne ya bondia mmoja

ambapo ukiwa kama mpenzi au shabiki wa bondia mmojawapo unaweza kujifunza mambo mengi kupitia video hizo

DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika makutano ya barabara ya uhuru na msimbazi Dar es salaam kituo kikuu cha mawakala wa magazeti mbalimbal;i masaa 24 zaidi unaweza kuwasiliana moja kwa moja na kocha Super D kwa namba za simu 0787406938 AU 0754406938

BONDIA VICENT MBILINYI 'SUGU' AJIFUA KUMKABILI KEIS AMAL MEI 30


 Na Mwandishi Wetu

BONDIA Vicent Mbilinyi 'Sugu'  ameingia kambini kwa ajili ya mpambano wake mwingine utakaofanyika mei 30 katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba ambapo atakabiliana na Keis Amal kutoka Mzazi GYM

bondia huyo anaenolewa na Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ameingia kambini jana kwa ajili ya mpambano uho wa raundi sita ambapo siku hiyo mpambano mkubwa utakuwa ni kati ya bondia Fransic Cheka na Kiatchai Singwancha . kutoka
Thailand


mpambano utakaokuwa wa raundi kumi promota wa mpambano uho Kaike Siraju aliongeza kwa kusema kuwa siku hiyo pia kutakuwa na mapambano mbalimbali ya utangulizi ya kuvutia ambayo yatatajwa wakati ukifika 

hata hivyo amendelea kumkumbusha Cheka kuwa afanye mazoezi ya kutosha na akumbuke bondia anaekuja kucheza nae ni zaidi aliwo kutana nawo awali

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha
Bondia Vicent Mbilinyi 'Sugu' kushoto akipambana na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa mazoezi ya Mbilinyi kujiandaa kupambana na Keis Amal  mpambano utakaofanyika mei 30 katika ukumbi wa P.T.A sabasaba Dar es salaam Picha na
SUPER D BOXING NEWS


Super D Boxing Coach
Email.superdboxingcoach@gmail.com
www.burudan.blogspot.com
www.superdboxingcoach.blogspot.com
 Mob;+255787 406938
        +255713406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

Friday, April 10, 2015

NGUMI KUFANYIKA MKWAKWANI TANGA MEI 2


Bondia Alen Kamote wa Tanga atapanda uringoni mei 2 katika uwanja wa mkwakwani tanga kukabiliana na Emilio Norfat katika mpambano wa raundi 12 mbali na mpambano uho siku hiyo pia kutakuwa na mapambano mengine makala moja ya mpambano wenye mvuto zaidi ni kati ya bondia mwenye makazi yake mkoa wa Morogoro Cosmas Cheka atakaekabiliana na Said Mundi kutoa mkoa wa tanga
 
promota wa mpambano uho Ally Mwazoa aliongeza kwa kusema mbali na mapambano hayo kutakuwa na mapambano mengine yatakayowakutanisha  Jacobo Maganga na Fadhili Kea wakati Juma Mustafa akipamana na Ally Magoma uku Saimon Zabroni akioneshana umwamba na Hamisi Mwakinyo
na Jumanne Mohamed na Bakari Shendekwa na Zuber Kitandura na Rajabu Mahoja

mpambano uho unafanyika mkoa wa tanga baada ya kutopata burudani ya mchezo wa masumbwi kwa kipindi cha mda mrefu kidongo hivyo mpambano uho utafuraiwa na wakati wa Tanga na vitongoji vyake

siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za ngumi  mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

“Ninatarajia kuwepo kwa ajili ya kuwauzia DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika Mpambano  ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi”, alisema Super D

Mfahamu bondia pekee aliyewahi kumchapa Mayweather


NA MWANDISHI WETU
KUNA kitu wengi hawakielewi kuhusu Floyd Mayweather Jr. Tangu aanze kucheza ngumi za kulipwa hajawahi kupoteza, lakini tangu aanze kupanda ulingoni amepigwa mara moja tu na aliyeifanya hii kazi anapatikana katika mji wa Pazardzhik, Bulgaria. Unamjua ni nani?
Anaitwa Serafim Rorodov. Kwa kumtazama usoni hivi sasa inaweza ikawa ngumu kwako kuamini ulichokisoma hapo juu, lakini ukiyapitia vizuri mashindano ya Olympic mwaka 1996 yaliyofanyika Atlanta, Marekani utatikisa kichwa chako na kutoa heshima kwake.
Kwa sasa Todorov anaishi pamoja na
 mke, mtoto wake wa kiume na binti wake wa kike ambaye ni mjamzito. Maisha yake ni ya chini mno na hakuna kilichobora kwenye maisha yake zaidi ya rekodi ya kumchapa kisiki Floyd Mayweather japo mwenyewe amekuwa akichukizwa mara kwa mara kila anapokumbushiwa suala hili. Kwanini? Ilikuwa akampiga Mayweather? Makala haya yamekusanya majibu yote ya maswali hayo.
Ushindi wa Todorov alioupata enzi hizo akiwa na umri wa miaka 27 mbele ya Mayweather aliyekuwa na miaka 19 kwenye pambano la uzito mwepesi katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Olympic mwaka 1996, ndio pigano la mwisho Mayweather kupoteza ulingoni.
Miezi michache baadae baada ya kichapo hiko, Mayweather aliachana na ngumi za ridhaa na kuingia kwenye mapambano ya ngumi za kulipwa alipotengeneza rekodi ya kucheza michezo 47 bila kupoteza mpaka sasa na kutengeneza mamilioni ya pesa.
Kwa Todorov mwenye miaka 45 sasa, kuna tofauti kubwa ya kimaisha baina yake na Mayweather tangu mara ya mwisho wawili hawa walipopambana.
Mayweather aliyepoteza pambano anakadiriwa kuwa na utajiri wa dola milioni 280 wakati Todarov aliyeibuka kidedea hamiliki hata ‘flat screen’ sebuleni kwake. Hali hii ndio inayomtia simanzi Todorov kila siku.
Kwa kipindi kirefu mashabiki wa masumbwi hususani Wamerakani wamekuwa wakiuponda ushindi wa Todorov wakidai kuwa majaji wa pambano lao walimpendelea.
Lakini hili ni kama halimuumizi kichwa sana Todorov, kinachoonekana kumtatiza ni namna maisha yake yalivyobadilika tangu alipotoa kichapo hiko cha Kihistoria miaka 19 iliyopita.
Mikosi ilianza kumuandama baada ya pambano lile ambapo Todorov alitemwa na shirikisho la masumbwi hali iliyomfanya ashindwe kuliwakilisha taifa lake katika mapambano ya kimataifa.
Wakati leo hii Mayweather akijiandaa kupokea dola milioni 180 kwa pambano lake dhidi ya Pacquiao, Todorov anaishi kwa kutegemea pensheni ya dola 435 kwa mwezi.
Hali hii inamfanya Todorov, binadamu pekee aliyemchapa Mayweather ulingoni kuamka kila siku asubuhi na kujuta kwanini alishinda pambano hilo.
“Alikuwa na miaka 19 kumbuka, uzoefu wangu ulingoni ulikuwa mkubwa zaidi yake. Nilishawachapa mabondia mbalimbali kutoka Urusi, Cuba, Ujerumani, Ufaransa na Uingereza” alisema Todorov
“ Lilikuwa pambano zuri na la kuvutia, unahitaji kuwa vizuri zaidi ya mwenzako ili kupata ushindi. Mimi nilikuwa vizuri kwa siku ile”aliongeza bondia huyo.
Todorov bingwa mara mbili wa Ulaya katika ngumi za ridhaa alianza kujifunza ngumi akiwa na miaka 8 akipata mafunzo kutoka kwa mjomba wake katika kitongoji cha Peshtera, kusini mwa jiji la Pazardzhik, Bulgaria.
Udhaifu pekee wa Todorov ambao kocha wake Georgi Stoimenov, aliueleza ni kuwa, mbali na uhodari wa bondia huyo ulingoni ni mbovu sana kwa wanawake.
“ Tukiwa kwenye mashindano, kocha unatakiwa kulala chumba tofauti na kijana wako. Lakini kwangu ilikuwa lazima nilale nje ya mlango wa Todorov kwa ajili ya kumlinda” alisema kocha huyo.
Stoimenov aliongeza kuwa kuna kipindi alilazimika kumfungia Todorov kwa nje, lakini alipoamka asubuhi alimkuta ametoroka chumbani kwa kupitia dirishani.
Unajua Stoimenov alimpatia wapi Todorov? “ alimkuta mklai huyo akiwa amejifungia kwenye kambi ya wanawake waliokuwa wakishiriki riadha.
Hatahivyo Todorov anakubali kuwa Mayweather ni bondia mkali lakini kwa upande wake hakutumia muda mwingi kumchunguza kabla ya kupanda nae ulingoni.
“ Nilikuwa bondia niliyekamilika sana. Sikuwa na muda kumsoma. Nilipomtazama ulingoni kwenye pambano lake la robo fainali, ilitosha sana kwangu kuona udhaifu wake na kumchapa” alisema Todorov.
“ Lakini ukweli halikuwa pambano la kawaida, nilimpiga mmoja kati ya mabondia bora kabisa ulimwenguni.” Aliongeza Todorov.
Kuhusu hali ya maisha yake ilivyo hivi sasa, Todorov amekiri kuvurugika na akichukua zaidi kuwa na rekodi hiyo ambayo kwa sasa dunia inamtazama kwa sana.
“ Kwenye maisha, ni kawaida kushinda vitu vichache na kushindwa na vitu vingi. Nachukia na ninajutia kuwa na rekodi ya aina hii kwenye maisha yangu” alisema Todorov.
Sababu kubwa inayodaiwa kusababisha mapromota kumkumbia Todorov na kuanza kuweka pesa kwa Mayweather, ni kitendo cha mkali huyo kudengua mara kwa mara katika kusaini mikataba.
Lakini mmoja wa watu waliokuwa wakifanya kazi na bondia huyu, Angel Angelov, anasema kuwa maisha ya Todorov yalibalika tangu alipopokea kichapo kutoka kwa Kamsing.
Angel anaamini kuwa Todorov bado ana mawazo ya pambano lile ambalo aliamini ni wazi kuwa majaji walimkandamiza ili apoteze pambano lile.
“ Nakumbuka Todorov alikuwa karibu ya kuchanganyikiwa baada ya raundi ya kwanza ya pambano lile. Alifoka kwa hasira kwa kocha wake akimwambia kuwa majaji hawahesabu ngumi zake” alisema Angel ambapo mwisho wa siku Todorov alipoteza pambano hilo kwa pointi 8-5.
Baada ya kichapo hiko, Todorov alitumia siku mbili akiwa hotelini akisubiri ndege ya kumrudisha kwako.
“ Sitaacha kunywa pombe kwa maisha yangu yote, na ninataka kifo change kinikute nikiwa na pombe” alisema Todorov anayehisi maisha yake yametawaliwa na usaliti.
Kwa sasa Todorov anaishi katika kibanda kilichozungukwa na mashamba ya ya ndizi eneo linalofahamika zaidi kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya nchini Bulgaria.
“ Kuna mambo ya ajabu zaidi mahala hapa, mambo mengi mabaya yanaendelea mahala hapa. Sipendezwi na maisha haya. Hakuna sehemu za mafunzo ya ngumi za kutosha, siongei na watu wengi wa hapa na kwa sasa sihitaji zaidi marafiki. Nahitaji kupumzika tu” alisema Todorov.
Todorov anaamini kama angepoteza pambano lile la Mayweather, angeendelea vyema na mchezo huo kama alivyofanya kwenye michuano ya Olympic.
Pia anaamini kabisa asingepata nafasi ya kuishi Marekani alikokutana na fedheha ya kichapo cha uonevu mbele ya Kamsing. “ Yameshatokea, na nimeshasahau. Kwa sasa nahitaji kuishi na kusahau yaliopita. Kuna mambo ya kipuuzi niliyafanya na nilipokuja kugundua tayari nilishadumbukia shimoni”
Kuhusu rekodi yake ya kumchapa Mayweather kama bado watu wanaikumbuka, Todorov alisema “ Wanakumbuka, lakini huwa sipendi kusikia ninapopota mtaani watu wakisema, Yule ndiye mtu aliyewahi kumpiga Mayweather”.