Tangazo

Pages

Saturday, June 29, 2013

SIMULIZI ZA MZEE MADIBA ;MANDELA BONDIA ALIPOKUTANA NA BONDIA


2 1bd4f
Ndugu zangu,
Kuna simulizi nyingi za Mzee wetu Madiba. Hakika, Nelson Mandela hajawahi kuwa mpenda makuu.
Mzee Mandela yuko simple sana, ni tangu enzi za ujana wake. Lakini, kuna ambao hawajui kuwa Mandela anapenda sana mchezo wa ngumi, na kuwa , yeye mwenyewe aliwahi kuwa bondia.
Kuna wakati akiwa Ikulu kama Rais, Mandela alipata habari za bondia wa Afrika Kusini aliyetwaa taji la  kimataifa. Mandela alifurahishwa sana na habari hizo. Akataka ampongeze mwenyewe bondia  huyo.
Siku moja akiwa na wasaidizi wachache sana, Mandela alikwenda hadi nyumbani kwa bondia huyo. 
Alihakikisha kuwa
bundia huyo yuko nyumbani kwake. Alipofika, Mandela aliwaambia wasaidizi wake wakamwambie bondia huyo kuwa nje kuna mtu anayehoji ubingwa wake. 
 Wamwambie kuwa  mtu huyo ( Nelson Mandela) anadai kuwa yeye ndiye bingwa wa uzito huo katika Afrika Kusini ( Nelson Mandela!) Kwamba anataka mkutane mpange siku ya kupigana ili apatikane mshindi halali wa taji hilo.
Basi, bondia yule akapokea habari hizo na akatamani sana amwone huyo anayedai kuwa ana ubavu wa kupambana naye.
Alipotoka nje akakutana na Nelson Mandela akiwa amesimama getini na amekunja ngumi yake. Akatania; “ Nimekuja kwako tuzipige ili dunia imjue bingwa halisi!”
Ikawa ni furaha kubwa kwa bondia yule. Hakuamini macho yake. Kuwa Rais wan chi amekuja nyumbani kwake kumpongeza.  Kumpongeza kwa jambo kubwa alilolifanya kwa taifa la Afrika Kusini. 
Na Mandela akawa tayari kuingia nyumbani kwa bondia huyo na kunywa nae chai!
What a Great Leader Of Africa! Yes, Nelson Mandela!
Maggid Mjengwa,
Iringa.

Thursday, June 27, 2013

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA BFT KUFANYIKA JULAI 7 MWAKA HUU





TANZANIA BOXING NEWS: UCHAGUZI BFT JULAI 7


Uchaguzi wa viongozi wa BFT uliopangwa Kufanyika tarehe 7/7/2013 jijini Mwanza, utafanyika kwa tarehe hiyo kama ulivyopangwa.

Kikao cha kamati ya utendaji ya BFT kilichofanyika juzi katika  ofisi za BFT kikiongozwa na Rais wa shirikisho Joan Minja kimesisitiza kuwa uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa na haujaairishwa kama baadhi ya kikundi 
cha watu wachache wanaojiita wadau wanavyoweka pingamizi na kupotosha  
kwa kuwashawishi wajumbe wa mkutanao mkuu hasa kutoka mikoani 
kutohudhuria mkutano huo wa uchaguzi,kwa manufaa yao binafsi na 
kinyume na katiba yetu.

Upotoshaji huo unafanywa na  Akaroly Godfrey aliyekuwa  kiongozi katika uongozi uliojiudhuru kutokana na kashfa za kusafirisha madawa ya kulevya 
na kusababisha Tanzania kufutwa uanachama na chama cha ngumi cha 
dunia (AIBA) na kusababisha  kutoshiriki mashindano,mikutano na 
shughuri zote za kimataifa za chama cha ngumi cha Dunia AIBA. Naomba 
wadau na serikali kuwa makini na watu wanaoshawishi kwa lengo la 
masilahi yao binafsi na kusababisha michezo kudolola badala ya kusonga 
mbele.

Fomu za uchaguzi zilishaanza kutolewa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) toka tarehe 4//2013 na zitaendelea kutolewa hadi tarehe 4/7/2013 jijini 
Mwanza na tarehe hiyo  ndio itakuwa siku ya mwisho ya kuchukua na 
kurudisha fomu, tarehe 5/7/2013 itatakuwa siku ya usaili na utafanyika jijini mwanza, tarehe 6/7/2013 kupitia pingamizi na kuzitolea maamuzi na tarehe 7/7/2013 ndio siku ya uchaguzi.
Kimsingi taratibu zote za kuitisha uchaguzi kwa mujibu wa katiba yetu zimezingatiwa na zimekamilika.

Aidha BFT inatoa tamko kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu kufika katika 
uchaguzi uchaguzi, ili kupata viongozi halali kwa mujibu wa katiba, 
waendelee na shughuri za kuendeleza mchezo wa ndondi na kuaandaa timu 
ya taifa kushiriki katika mashindano ya Afrika nchini Mauritius Sept. 2013

BFT inatoa wito kwa watu wote wenye sifa, nia, moyo na uwezo wa kuongoza wajitokeze kuchukua fomu za kugombea uongozi kwani wakati ndio huu.

Wednesday, June 26, 2013

MUDY MATUMLA AJITAPA KUMCHAKAZA MPINZANI WAKE JULAI 6 DDC KEKO


MUDY MATUMLA

Akizungumza na mwandishi wetu mwandaaji wa mpambano huo Shabani Adios 'Mwaya mwaya' amesema mpambano huo utasindikizwa na mabondia mbalimbali wanaotamba katika masumbwi

Mabondia hawo ni Shafii Ramadhani atakayemenyana na Juma Fundi huku Swaleh Mkalekwa akipambana na Cosmas Kibuga

mpambano huo unaotarajiwa kuwa wa kukata na shoka wa raundi sita umekuwa wa kusisimua na kuzagaa katika vinywa vya mashabiki wa mchezo huo

Huku bondia Mohamed Matumla akimtahadhalisha mpinzani wake kuwa siku hiyo ato kuwa na msalia mtume kwani kawaida yake inajulikana Matumla mpaka sasa amepambana mapambano 13 akidroo matatu na kushinda 10 ata hivyo ame sisitiza kumuhangamiza mpinzani wake mapema kadri iwezekanavyo na kuwaomba wapenzi wa mchezo huo waje mapema kushudia anavyo mmaliza vinginevyo watakosa uhondo wa masumbwi Mbali na kuwepo na mpambano huo Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' atasambaza DVD za mafunzo ya mchezo wa masumbwi
 
CD hizo zilizotengenezwa kwa umakini wa ali ya juu ambazo zitakuwa chachu kwa ajili ya kuvutia wapenzi na mashabiki mbalimbali kujua mchezo wa masumbi wakiwa wanangalia live mana DVD hizo zina maelekezo ya sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika masumbwi

DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au unaweza kuzipata jengo la Azam lililopo mtaa wa Msimbazi karibu na kituo cha Polisi Post Gelezani kwingine ni GYM ya Amana iliyopo Ilala au unaweza kuwasiliana na kocha kwa simu 0713406938 ili uweze kupata dvd hizo kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo
 
katika mchezo mbalimbali ya masumbwi kutakuwa na CD na DVD za mafunzo ya mchezo
huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo katika CD na DVD


mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali 
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

UCHAGUZI BFT KUFANYIKA MWANZA