Tangazo

Pages

Monday, December 31, 2012

MPAMBANO WA MASUMBWI KUPIGWA Janual 27 katika ukumbi wa wa CCM Tandare



SUPER D BOXING COACH AKIMWELEKEZA KING CLASS MAWE
Mabondia Hassan Mandulla na Jems Martin wanatarajia kupanda ulingoni Janual 27 katika ukumbi wa wa CCM Tandare Dar es salaam akizungumza mpambano huo mwandaaji Waziri Rosta
amesema kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi yakiwemo ya mabondia maarufu na chipkizi alisema mapambano ya utangulizi ni Fadhiri Majia na Anton Matiasi mpambano mwingine

Utawakutanisha Shabani Kilumbelumbe na Mwaite Juma na Chaeles Mashali atavaana na Adam Ngange, Julias Noro atapambana na Abdallah Luwajempambano mwingine utawakutanisha Rajabu Tumaini na Daudi Anton na Rashid Mohamed Atavaana na Eliman Richard wakati Rashid Hamisi atamvaa Omary Shabani

Super D, alisema katika mpambano huo atasambaza DVD zake mpya tofauti na kanda yake ya awali iliyokwenda kwa SUPER D BOXING COACH, DVD za sasa zimeandaliwa kisasa na zikiwa na mchanganyiko wa ‘clips’ za michezo ya nyota wa Dunia katika kuwafunza watu namna ya kupigana ngumi.Super D, alisema mbali na michezo ya nyota hao wa Dunia akiwemo Manny Pacquio,Juan Emanuel Marquez, Floyd Maywether, Roy Jones na wakali wengine DVD hizo zina.

 michezo
ya tamasha lao la ngumi wanaloendesha kwa kushirikiana na kocha mkongwe Habibi Kinyogoli.”katika muendelezo wa kuwafunza watu ngumi kwa njia rahisi, nimetoa dvd pamoja na CD nyingine tofauti zilizokusanya michezo ya mabingwa wa dunia na mafunzo ya ngumi tunayoendesha kupitia tamasha letu na Kinyogoli Foundition ” alisema.


 Super D ambae ni kocha wa timu ya ngumi ya Ashanti pamoja na timu ya mkoa wa Ilala kimichezo alisema anamini kupitia njia  hii watu wengi wenye kupenda kujifunza mchezo wa ngumi kwa kuangalia mbinu na ufundi katika mchezo huo kupitia michezo ya mabondia waliopo kwenye dvd hizo. 

 
Aliongeza kuwa, mbali na dvd hizo bado wanaitajika vijana wenye vipaji kujitokeza kuja kushiriki katika mazoezi ya ngumi ili wajiunge na wenzao wa
timu ya Ashanti na Amana kujifunza ‘live’ chini ya makocha Habibu Kinyogoli, Kondo Nassoro, na yeye mwenyewe Super D na wengine wanaowanoa vijana

TASWA YAFANYA MKUTANO WA SIKUMOJA NA WANACHAMAWAKE BAGAMOYO MKOANI PWANI.




Baazi ya wanachama wa TASWA wakiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete Picha na www.burudan.blogspot.com
Katibu Mkuu wa TASWA Amir Muhando akizungumza katika mkutano Mkuu leo Picha na www.burudan.blogspot.com
Baazi ya wanachama wa TASWA wakiburudika katika hotel kubwa mjini bagamoyo ya Kiromo view Hotel jana usiku kutoka kushoto ni Somoe Ng'itu, Hadija Khalili' Zena Chande na Angela Msangi
Shafii Dauda akiwa na dada Asha Muhaji picha na www.burudan.blogspot.com
Mmiliki wa blog ya Bongo Staz Mahmud Zubeir kulia akizungumza na Wiliam Chiwango na Salim Said Salim
 Mjumbe wa mkutano huo, Rajabu Mhamila 'Super D' akijitambulisha kwa mgeni rasmi
Baazi ya wanachama wa TASWA wakisikiliza mada mbalimbali
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto  akiwa na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete walipokutana katika mkutano mkuu wa Taswa
Baazi ya wanachama wa TASWA wakiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete Picha na www.burudan.blogspot.com

Mmoja wa waandishi wa habari Egbert Mkoko akitoa salamu kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa TASWA Picha na www.burudan.blogspot.com
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto  akiwa na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete pamoja na mweka hazini wa TASWA Sultani Sekilo walipokutana katika mkutano mkuu wa Taswa
Mwanachama wa Taswa Saleh Ally akichangia mada wakati wa mkutano huo picha na www.burudan.blogspot.com
Katibu Mkuu wa TASWA Amir Muhando akitoa neno la shuklani kwa wajumbe waliohuzulia mkutano wakati wa kufunga mkutano huo Picha na www.burudan.blogspot.com
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto  akiwa na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete pamoja na mweka hazini wa TASWA Sultani Sekilo walipokutana katika mkutano mkuu wa Taswa
Baazi ya wanachama wa TASWA wakiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete Picha na www.burudan.blogspot.com

Saturday, December 29, 2012

ARUSHA KUWA MAKAO MAKUU YA CHAMA CHA NGUMI ZA KULIPWA AFRIKA YA MASHARIKI NA KATI (ECAPBA).





 Chama cha Ngumi za Kulipwa Cha Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBA) kimepata nyumbani baada ya Mstahiki Meya wa jiji la Arusha  Mh. Gaudence Lyimo kuomba kihamie Arusha ili kiweze kukaa karibu na “Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, EAC”Rais wa ECAPBA Onesmo Ngowi alimhakikishia mstahiki meya kuwa ECAPBA itahamishia makao yake makuu katika jiji la Arusha. Kwa sasa ECAPBA ina makao yake makuu katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi.
 Juhudi za Mstahiki Meya Gaudence Lyimo za kukuza michezo na kukuza utalii katika jiji la Arusha ni moja ya sababu zilizomfanya rais wa ECAPBA kuamua kuhamishia makao makuu katika jiji la Arusha.
 Uamuzi huo uliungwa mkono na mmoja wa wanachama wa  ECAPBA bw. Daudi Chikwanje ambaye ndiye Katibu Mkuu wa Chama Cha Ngumi za Kulipwa Cha Malawi!
 Nchi ya Malawi ni mwanachama wa ECAPBA pamoja na Kenya, Zambia, Ethiopia, Burundi, Sudan ya Kusini, DRC, Rwanda, Uganda na Sudan.
 ECAPBA inaratibu ubingwa unaojulikana kama ECAPBF ambao unawapa mabondia wa ukanda huu kuwa mabingwa imara wa ngumi Afrika

Thursday, December 27, 2012

CHEKA AWAPA RAHA MASHABIKI WA NGUMI JIJI LA ARUSHA




Meya wa jiji la Arusha Gaudence Lyimo na rais wa TPBC Onesmo Ngowi wakimvisha mkanda Francis Cheka

Francis Cheka akiongea na waandishi wa Habari baada ya pambano kumalizika


Frincis Cheka akikwepa konde la Chimwemwe

Jaji Boniface Wambura akitafakari kitu kabla mpambano kuanza




Bondia Francis Cheka leo ametwaa ubingwa wa IBF Afrika baada ya kumpiga kwa pointi bondia toka Malawi Chiotka Chimwemwe kwenye pambano la raundi 12 lililofanyika kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha.

Majaji wa pambano hilo ambao walikuwa watatu walitoa maksi kama ifuatavyo: David Chikwanje alimpa Cheka pointi 112/114 za Chimwemwe, Boniface Wambura alimpa Cheka pointi  118/114 za Chimwemwe na James Ligongo alimpa Cheka pointi  120/115 za Chimwemwe


Cheka ambaye alipigwa konde la haja likasababishwa kuchanika katikati ya paji la uso raundi ya pili aliweza kuhimili kumaliza raundi zote huku akitibiwa kila saa.


Baada ya Mpambano kumalizika Cheka allisema anashukuru ameshinda ila mpambano ulikuwa mgumu sana kwake na alikiri hajakutana na bondia mkali kama Chimwemwe kwa karibuni.

 "Nashukuru nimeshinda ila nimeshinda kwa bahati kwani bondia niliyekutana naye ni bondia mzuri kwani angeweza kushinda ila alikosa mbinu chache tu", alisema Cheka.

Naye bondia Chiotka Chimwemwe alikubali matokeo na kusema ni mara yake ya kwanza kupigana nje ya nchi yake  hivyo amechukulia kama changamoto kwake.


Cheka ameweza kutwaa Ubingwa wa IBF Afrika baada ya kunyang'anywa kwa kushindwa kuutetea kwa muda na akaenda kucheza na Karama Nyilawila ubingwa wa UBO ambao pia alimpiga Nyilawila.


Naye Meya wa jijini la Arusha  Gaudence Lyimo alimpongeza promota wa pambano hilo Andrew George na Rais wa TPBC Onesmo Ngowi kwa kuleta pambano hilo la kimataifa Arusha na kusema atashirikiana nao kuwahakikisha anainua mchezo wa ngumi Arusha.


"Nawapongeza walioleta pambano hili Arusha na wnawaahidi tutakuwa tukishirikiana bega kwa bega kuahakikisha tunainua mchezo wa ngumi Arusha", alisema Meya.

SAID YAZIDU KUCHEZA KESHO UK


Nick Klappert WHO WILL FIGHT Said Yazidu, Chaurembo Palasa WHO WILL FIGHT Ashley Treasure Theophane [ FAR RIGHT ], PROMOTER Raymond Goy , Said Yazidu THEN Ashley Treasure Theophane. READY FOR 28.12.2012 LUXEMBOURG CLASH FOR TITLES.

IBF YAMPONGEZA BINGWA MPYA WA AFRIKA, GHUBA YA UAJEMI NA MASHARIKI YA KATI

TAARIFA KW AVYOMBO VYA HABARI

TAREHE 27/12/2012

Shirilisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limepongeza bingwa mpya wa uzito wa Super Middle katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati, Mtanzania Francis Cheka.

Katika barua yake aliyomtumia Francis Cheka ya tarehe 28/12/2012 Mwenyekiti wa kamati ya Ubingwa wa IBF/USBA Lindsey Tucker alisema "Tunachukua fursa hii kukutakia maisha na mafanikio mazuri kama bingwa wa IBF na kumhimiza kuishi kama bingwa". Cheka atatakiwa kutetea taji lake katika kipindi cha miezi sita kufikia mwezi wa 6 mwakani dhidi ya mpinzani ambaye ana rekodi ya mapambano yasiyopungua 15 na mengi awe ameyashinda hususan mapambano mawili ya mwisho.

Aidha IBF inampongeza bondia Chiotcha Chimwemwe kutoka Malawi kwa ushupavu wake na ushindani mzuri katika pambano hilo lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid katika jiji la Arusha tarehe 26 Desemba, 2012.


Imetolewa na:


Onesmo A.M. Ngowi
Rais
IBF/USBA Afrka, Ghuba ya Uajemi an Mashariki ya Kati



CHIOTCHA AONJA MACHUNGU YA CHEKA

Bondia kutoka Jamhuri ya watu wa Malawi Chiotcha Chimwemwe alionja machungu ya Mtanzania Francis Cheka katika mpambano wao uliopewa jina na “Vita vya Ziwa Nyasa” tarehe 26 Desemba 2012 siku ya Boxing Day jijini Arusha.

Ulikuwa ni mpambano wa mwaka ambao bondia Francis Cheka nusura aupoteze katika raundi ya pili wakati konde zito la kushoto la kapteni Usu kutoka katika jeshi la jamhuri ya watu wa Malawi, Chiotcha lilipompeleka chini na kuinuka kwa msaaada wa kamba za ulingo.

Konde hilo zito lilifungua mpasuko mkubwa katika paji la Cheka na hivyo kuleta wasiwasi kwa mashabiki zaidi ya elfu 10 waliofurika katika uwanja wa Sheikh Amri Abed kumshughudia Cheka akipambana kiume kwelikweli.

Raundi ya kwanza mpaka ya nne Chiotcha alikuwa anamiliki mpambano huo na makonde mazito ya mkono wake wa kushoto kwani anatumia staili ya South Paw inayomlazimu kutanguliza mbele mguu wa kulia.

Ni katika raundi ya sita ambako Cheka aliweza kubadilisha mwelekeo wa mpambano kwa kuanza kumwadhibu Chiotcha na makonde mazito ya kombinasheni yaliyomfanya Mmalawi huyo kumkumbatia bila mafanikio Mtanzania huyo asiyepigika.

Cheka aliwanyanyua mashabiki waliojaa uwanjani wakiongozwa na Mstahiki Meya wa jiji la Arusha, Mh. Gaudence Lyimo alipompiga bila huruma Chiotcha na kumlazimu refarii wa kimataifa wa mpambano huo Nemes Kavishe wa Tanzania kumwonya kutomshika Cheka kama vile anapigana mieleka.,

Juhudi za Chiotcha kujisalimisha kwa kumkumbatia Cheka hazikuzaa matunda kwani aliendelea kupewa mkong’oto na mwana huyo wa Kitanzania aliyejizolea sifa kemkem kwa kuwapiga wapinzani wake.

Mashabiki wengi walinyanyuka katika viti vyao katika raundi ya 12 ya lala salama wakati Cheka alipodhihirisha kweli ni bondia asiyepigika kwa kumpiga makonde mazito kichwani Chiotcha na kumfanya apepesuke kila mara.

Katika mchezo huo ulioandaliwa na kampuni ya Green Hills (T) Investment ya jijini Dar-Es-Salaam inayomilikiwa na bingwa wa zamani wa taifa Andrew George, mabondia wa mapambano ya utanguliizi walikuwa wa ngumi za ridhaa kutoka katika jiji la Arusha.

Mpambano huo ulisimamiwa na Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi akisaidiwa na Kamishna wa TPBC kutoka Jiji la Arusha bw. Roman Chuwa.

Refarii alikuwa Nemes Kavishe kutoka Tanzania wakati majaji walikuwa: Daudi Chikwanje kutoka Malawi, Boniface Wambura kutoka Tanzania na Galous Ligongo kutoka Tanzania.


Imetolewa na

Uongozi, TPBC

Wednesday, December 26, 2012

NDONGA ZA MWAKA DAR LIVE: WATANZANIA WATOA KICHAPO KWA WAPINZANI WAO



Mada Maugo (kushoto) akimshushia kichapo bondia Yiga Juma (Uganda) wakati wa mpambano wao.
Bondia Mbwana Matumla (kulia) akitupiana makonde na bondia David Charanga kutoka Kenya.
Bondia David Charanga kutoka Kenya (kulia) akienda chini baada ya kupokea konde kutoka kwa Mbwana Matumla.
David Charanga kutoka Kenya (kulia) akimkabili bondia Mbwana Matumla wakati wa mpambano wao jana.
--
Mabondia wa Tanzania jana waling'ara katika mapambano yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Zakhem. Bondia maarufu nchini, Mada Maugo alimchapa Yiga Juma kutoka Uganda raundi ya kwanza kwa ‘Knock Out’. Katika hali iliyoonesha kuwa siku ya vichapo kwa wageni, pambano lingine ambalo bondia Mbwana Matumla alipambana na bondia kutoka Kenya, David Charanga lililokuwa la raundi nane, Matumla aliibuka kidedea katika raundi zote nane na kumfanya aibuke na ushindi wa kishindo.
(PICHA NA ISSA MNALLY NA RICHARD
Bondia Mada Maugo (Tanzania) akitangazwa mshindi baada ya kumtwanga bondia Yiga Juma (Uganda) kwa KO raundi ya kwanza.
Bondia Mbwana Matumla (Tanzania) akitangazwa mshindi baada ya kumpa kichapo bondia David Charanga (Kenya).

FRANCIS CHEKA NA CHIOTCHA CHIMWEMWE WAPIMA UZITO KUZICHAPA LEO SHEIKH AMRI ABEID KUWANIA MKANDA WA IBF


 Mabondia Francis Cheka (kushoto) na Chiokta Chimwemwe wakiwa wameshika mkanda watakaougombea muda mchache ujao jijini Arusha leo, wakati wa utambulisho wao na zoezi la kupima uzito.
 Bondia Francis Cheka akipima uzito

.
 Bondia Chiokta Chimwemwe akipima uzito.

Mabondia Francis Cheka (kushoto) na Chiotcha Chimwemwe, kupigana baada ya kupima uzito na kucheki afya leo asubuhi.
***************************************
Mafahali mawili wanaotegemea kuzichapa tarehe 26, 2012 kugombea mkanda wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Francis Cheka na Mmalawi Chiotcha Chimwemwe nusura wazichape kavukavu wakati wa upimaji uzito na mkutano wa waandishi wa habari katika hoteli ya nyota 5 yaNaura Springs, jijini Arusha jana tarehe 25 Desemba 2012.



Hii ni mara ya kwanza kwa ngumi za kulipwa kupewa hadhi kubwa kama hiyo ya kuwekwa kwenye hoteli ya nyota tano (5) hapa Tanzania.



Wawili hao walikuwa katika hoteli hiyo ya kifahari ya Naura Springs inayomilikiwa na bwana Felix Mrema anayemiliki mahoteli lukuki katika jiji la Arusha na Moshi ambazo ni Naura Springs Hotel, Impala Hotel, Ngurudito Hotel, Impala Moshi na Livingstone Hotel za Moshi!



Mpambano huo uliopewa jina la “Vurumaini chini ya Mlima Meru”umekuwa ni gumzo katika jiji la Arusha, Moshi, Tanga, Dodoma, Manyara pamoja na nchi jirani za Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda na unaandaliwa na kampuni ya kizalendo ya Green Hills (T) Limited inayomilikiwa na bondia wa zamani wa taifa katika ngumi za ridhaa na kuloipwa George Andrew na familia yake.



Aidha, watalii wengi walioko katika jiji la Arusha wakati huu wa sikukuu ya Xmas wameonyesha nia zao za kuliangalia pambano hili na wengine wameshakata tiketi tayari kuingia katika ujwanja wa Sheik Amri Abeid kuwashughudia mafahali hao wawili wakitoana jasho.



Chiotcha mwana wa Chimwemwe mwanajeshi wa ngazi ya Luteini Usu katika jeshi la Malawi amepania kulibeba juu taifa lake lililoko pembezoni mwa ziwa Nyasa kwa kumwonyesha Francis Cheka kuwa ngumi zinaendana na ushupavu.



Chimwemwe anadai kuwa hakuja Tanzania kutalii kama walivyo watalii wengine bali alikuja kuwakilisha nchi yake aipendayo ya Malawi na kurudi kwao na mshipi wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati. Alisema kuwa kushinda kwake sio kitu cha kubahatisha ila ni uhakika.



Naye Francis mwana wa Cheka, Mtanzania aliyeipeperusha vyama bendera ya taifa hili katika mapambano mengi bila kuzivunja nyoyo za mashabiki wa ngumi nchini alisema kuwa “Mwache Mmalawi huyo ajifurahishe tu kwani hajui kinachongojea ulingoni”



Cheka aliyejizolea sifa kemkem kati ya mabondia wa kitanzania aliendelea kusema kuwa yeye sio mzungumzaji sana ila ngumi zake ndizo zitakazozungumza siku ya tareeh 26 Desemba, 2012.


“Asifikirie kuwa ngumi ni kupiga makelele tu na ukashinfa” alisema Chelka akimwangalia Chimwemwe wakati alipokuwa anajigamba kwa sifa kemkem!



Mpambano huo wa kukata na shoka unakuja wakati ambako Arusha imekuwa ni jiji na linataka kutumia mapambano mengi ya ngumi ya kimataifa kukuza hadhi ya jiji hilo kama “Geneva ya Afrika” kutokana na mandari yake na mikutano mingi ya kimataifa inayofanyika katika jiji hili.



Francis Cheka anakutana na Chimwemwe baada ya kuutema mkanda wake wa IBF wakati alipokutana na Karama Nyilawila kugombea mkanda mwingine mbali na IBF hivyo kuupoteza ubingwa wa IBF. Cheka amepania kuuchukua tena mshipi huo na kuudhihirishia ulimwengu kuwa yeye kweli ni moto wa kuotea mbali!



Mpambano huo utahudhuriwa na viongozi wengi wakiongozwa na Meya wa jiji la Arusha Mstahiki Gaudence Lyimo pamoja na wageni wengi wanaofanya kazi kwenye mashirika kadhaa ya kimataifa ikiwa ni pamoja na mahakama ya kimataifa ya wahalifu wa kivita wa Rwanda, Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na Kati, ILO, UNICEF, WFP na nyingine nyingi.



Aidha watalii wengi wameacha kwenda mbugani siku ya pambano ili washughudie wenyewe ni nani zaidi kati ya Cheka na Chimwemwe.,



Pamabano hilo linaratibiwa na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Nchini (TPBC) chini ya Rais wake Onesmo Ngowi na kupewa baraka zote na Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF).


Waamuzi wa pambano ni:


Onesmo Ngowi - Kamishna Mkuu, Roman Chuwa ambaye ndiye Kamishna wa TPBC mkoa wa Arusha –(Kamishna Mkuu Msaidizi), Nemes Kavishe (Refarii), Boniface Wambura – (Jaji), Gallous Ligongo –(Jaji), Mark Hatia –(Jaji).

NDONGA ZA MWAKA DAR LIVE: WATANZANIA WATOA KICHAPO KWA WAPINZANI WAO


Mada Maugo (kushoto) akimshushia kichapo bondia Yiga Juma (Uganda) wakati wa mpambano wao.
Bondia Mbwana Matumla (kulia) akitupiana makonde na bondia David Charanga kutoka Kenya.
Bondia David Charanga kutoka Kenya (kulia) akienda chini baada ya kupokea konde kutoka kwa Mbwana Matumla.
David Charanga kutoka Kenya (kulia) akimkabili bondia Mbwana Matumla wakati wa mpambano wao jana.
--
Mabondia wa Tanzania jana waling'ara katika mapambano yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Zakhem. Bondia maarufu nchini, Mada Maugo alimchapa Yiga Juma kutoka Uganda raundi ya kwanza kwa ‘Knock Out’. Katika hali iliyoonesha kuwa siku ya vichapo kwa wageni, pambano lingine ambalo bondia Mbwana Matumla alipambana na bondia kutoka Kenya, David Charanga lililokuwa la raundi nane, Matumla aliibuka kidedea katika raundi zote nane na kumfanya aibuke na ushindi wa kishindo.
(PICHA NA ISSA MNALLY NA RICHARD
Bondia Mada Maugo (Tanzania) akitangazwa mshindi baada ya kumtwanga bondia Yiga Juma (Uganda) kwa KO raundi ya kwanza.
Bondia Mbwana Matumla (Tanzania) akitangazwa mshindi baada ya kumpa kichapo bondia David Charanga (Kenya).

Monday, December 24, 2012

MABONDIA WA ‘NDONGA ZA MWAKA’ WAPIMA UZITO KWA MPAMBANO WA KESHO



Mabondia wote wakiwa katika picha ya pamoja.
MABONDIA watakaotwangana kesho ndani ya ukumbi wa Dar Live ulioko Mbagala wamepima uzito leo asubuhi katika ukumbi wa Hoteli ya Atriums, iliyoko Afrika Sana, Sinza, Dar es Salaam.
Mabondia hao ni Mada Maugo wa Tanzania, Iga Juma wa Uganda, Mbwana Matumla wa Tanzania na David Charanga kutoka Kenya, Wengine ni Chupaki Chipinda, atakayezipiga dhidi ya Bahati Mwafyele na mabondia wa kike Esther Kimbe na mpinzani wake Irene Kimaro.
(PICHA ZOTE NA ISSA MNALLY/GPL)

Mada Maugo akiwa na mpinzani wake toka Uganda, Iga Jumaa.
Mada Maugo akipimwa uzito.
Mbwana Matumla naye akifanya zoezi hilohilo.
Esther Kimbe akipima uzito.
Irene naye akiwa kwenye mashine ya kupimia uzito.
David Charanga akiwa juu ya mashine ya kupimia uzito.
Iga Juma akipima uzito