Tangazo

Pages

Thursday, March 7, 2013

Laila Ali 'She Bee Stingin'' BONDIA PEKEE WA KIKE ALIYECHUKUA KIWANGO CHA JUU CHA FEDHA KATIKA WANAMASUMBWI

Laila Ali Curtis Conway Curtis Jr.
Leila ali akiwa na mumewe Curtis Conway pamoja na mtoto wao
Kwa sasa unakadiriwa pia utajiri wake unafikia kiasi cha dola za kimarekani milioni kumi ambazo ni zaidi ya fedha za kitanzania bilioni 16, ambazo ambazo amezitengeneza kutoka katika mchezo wa masumbwi duniani,

Matangazo ya bihashara, pamoja na kazi ya uwanamitindo 
Kutokana na umaarufu wake katika masumbwi , alijikuta akipata mikataba mbalimbali mikubwa ya matangazo ya biashara  katika makampuni na maduka makubwa Duniani, kama maduka ya kuuza vyakula,nguo na vifaa vya michezo hali iliyompatia nafasi ya kujiongezea kipato chake kwa haraka  leila alianza kujihusisha na masumbwi akiwa na umri wa miaka 15, huku msaada wake mkubwa ukitokea kwa baba yake mzazi ambapo baada ya kuonesha uwezo wake kwa mda mfupi arianza kuingia kwenye mapambano ya kimataifa 



Baada ya kupata ubingwa huo mwaka 2005 aliweza kutoa ubingwa mwingine unaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la ngumi za wanawake ' IWBF kwa kumtwanga Nikki Eplion kwa K,O ya raundi ya nne katika uzito wa female super middleweight title 

Pamoja na uwezo huo, Wapo baadhi ya mabondia wa kike kama Vonda Ward, Leatitia, Robinson na Ann Wolfe wamekuwa wakilalamika kuwa Leila anawakwepa kwa kupangiwa vibonde na kuhofia kupigwa.

Licha ya kufanya vizuri kwenye mchezo wa masumbwi, mitindo na matangazo ya biashara kwenye runinga lakini mara kadhaa amekua akialikwa kwenye vituo mbalimbali vya runinga kwa ajili ya vipindi hali inayomfanya kukusanya kiasi kikubwa cha fedha 

Baadhi ya vipindi hivyo maarufu ni pamoja na agaeorgr Lpez, Dancing with the Stars, American Gladiators,Celebrity Family. The Early Show

Katika historia ya  maisha yake ya ndoa ,leila amesha olewa mara mbili ambapo kwa mara ya kwanza aliolewa na Johnny Mcclain Agost 27,2000,ambaye walikutana kwenye sharehe ya kuzaliwa baba yake mzazi Mohamed Ali wakati anatimiza umri wa miaka 57.

Kabla ya kuoanaMacClain ndiye aliyekuwa promota wake katika michezo ya ngumi za kulipwa jambo ambalo lilimsaidia kufanya vizuri katika mapambano yake yote ambayo ajapigwa wala kutoa droo ata mpambano mmoja akiwa na alama won 24 (KO 21) + lost 0 (KO 0) + drawn 0 = 24  

Baada ya kuoana mwaka 2000 walikuja kuhachana mwaka 2005. mwaka 2007, leila alifunga ndoa na Curtis Conway , ikiwa ni ndoa yake ya pili . wadadisi wa mambo ya kimapenzi wanaeleza kuwa kilichomfanya kuolewa tena ni kutokana na kuwa na mvuto wa kimapenzi alionao mwana dada huyo maili awapo ulingoni,

Leila amefanikiwa kupata watoto watatu akiwa na McClain ambao ni Leilani,Cameron na Kelton. Baada ya kuolewa tena alipata watoto wawili ambao ni Curtis Muhame Conway Aliyezaliwa mwaka 2008 na Sydney  mwaka 2011

Kwa sasa leila amestafu kucheza mchezo wa masumbwi tangu acheze mchezo wake wa mwisho Tareha 3 -2-2007  na Gwendolyn O'Neil na kufanikiwa kumpiga kwa K,O raundi ya kwanza na kutangazwa kuwa bingwa wa mikata miwili ya WBC female super middleweight title
WIBA Women's International Boxing Association super middleweight title
Ingawa kazi kubwa anayofanya kwa sasa ni kutangaza vipindi mbalimbali kwenye television pamoja na mitindo 
Moja ya mambo ambayo yalishangaza ulimwengu katika fani ya mitindo mwaka 2012 akiwa na mimba ya miezi 9, aliweza kushiriki kikamilifu katika maonesho ya mavadhi aliweza kuonesha umahiri wake kwenye jukwaa kwa kupita akiwa kwenye tamasha la mavazi lililofanyika jijini London Nchini Uingereza Novemba 20, 2012

Amestaafu akiwa na rekodi ya kutopigwa ata mchezo mmoja ambapo alicheza michezo  24 alishinda kwa  KO 21 ambapo mabondia watatu pekee ndio aliwashinda kwa point 
huyo ndio leila Muhamed Ali
kwa mahitaji ya DVD ZAKE KWA AJILI YA KUONA MAPAMBANO YAKE MBALIMBALI LIVE TUWASILIANE KUPITIA


Leila ali akiwa na mumewe Curtis Conway pamoja na mtoto wao


No comments:

Post a Comment