Tangazo

Pages

Saturday, March 23, 2013

CHEKA ADUNDWA KWA TKO NA Uensal Arik WA Germany

BONDIA Francis Cheka march 22 alichezea kichapo cha TKO ya raundi ya saba  katika mpambano wake wa IBF Inter-Continental super middleweight title  

lililofanyika katika ukumbi wa  Universal mjini Berlin, Germany mpambano huo uliokuwa wa raundi 12 ulikutwa unaishia katika raundi ya saba baada ya kupokea kichapo kutoka kwa bondia Uensal Arik 

  bondia huyo aliecheza won 18 (KO 18) + lost 1 (KO 1) + drawn 0 = 19 na kushinda kwa K,O yote ambapo amepigwa mpambano mmoja tu  bondia huyo ambaye ni Germany anaetamba kwa kwapiga watu mnamo raundi za awali tu Cheka amefanya kuwa mtu wa 18 wa kupigwa kwa K,O na bondia huyo

Francis Cheka anaetarajia kuzidunda na Thomas Mashali Mei Mosi mwaka huu katika ukumbi wa PTA sabasaba ameweka doa rekodi yake kwa kupigwa na anatazamiwa kupandisha upya rekodi yake kwa kumpiga bingwa wa Afrika Mashariki Thomas Mashali ili kudhilisha kwamba yeye bado mbabe kwa upande wa Tanzania Cheka mpaka sasa ana rekondi ya won 27 (KO 15) + lost 7 (KO 4) + drawn 1 = 35 

Mpambano huo wa Germany aliocheza Cheka ni mpambano ambao yeye alikwenda kuziba pengo la bondia ambaye alikuwa amepata matatizo katika mazoezi na kulazimika kuziba nafasi hiyo ili mpambano ufanyike mei mosi

Cheka atatetea mkanda wake wa IBF Continental Africa super middleweight title katika mpambano wa raundi 12

No comments:

Post a Comment