Tangazo

Pages

Sunday, September 11, 2011

VITALI AMTAKA HAYE AJIONGEZEE REKODI

BINGWA wa WBC uzito wa juu Duniani, Vitali Klitschko ametangaza nia yake ya kutaka kupambana na David Haye.
Vitali mwenye rekodi ya kushinda mapambano 42 (39 kwa 'ko) na kushindwa mawili, alisema kuwa anamtaka haye kwa sababu nia yake ni kucheza mapambano makubwa matatu kabla ya kustaafu.
Alisema kuwa anatamani kucheza na bingwa huyo wa zamani wa WBA ambaye anaamini atakapomchapa itamsaidia kuongeza rekodi yake
Haye anatarajia kupanda ulingoni tena Oktoba 31, ili arejeshe mikanda ya IBF,WBA NA WBO aliyopoteza kwa kaka yake Vitali Wladimir Klitschko

No comments:

Post a Comment