Tangazo

Pages

Monday, April 2, 2012

TIMU YA TAIFA YA NGUMI KUKABIDHIWA VIFAA VYA MAZOEZI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

YAH:-TIMU YA TAIFA YA NGUMI KUKABIDHIWA VIFAA VYA MAZOEZI NA     
               LAPF TAREHE 3/4/2012 SAA 4.00 KATIKA OFISI ZA LAPF MILLENIUM
                TOWER KIJITONYAMA.

Awali ya yote shirikisho la ngumi Tanzania (BFT) tunatoa shukrani za dhati kwa kwa shirika la LAPF kwa mara nyingine  kukubali kuipatia timu ya Taifa ya ngumi msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya maandalizi kushiriki mashindano  ya kufuzu kushiriki mashindano ya Olimpiki yatakayofanyika Casablanca Morocco Aprili 27/2012 na hatimaye mashindano ya Olimpiki Julai 2012 London Uingereza.
Zoezi hilo litafanyika kesho tarehe 03/14/2012 kuanzia saa 4.00 asubuhi  katika Ofisi za LAPF zilizopo jengo la Millennium Tower Kijitonyama.
Timu ya Taifa ya ngumi ipo kambini Kibaha katika shule ya Filbert Bayi ikiwa na jumla ya wachezaji kumi wa uzito wa kuanzia l/fly hadi super heavy ikiwa na jumla ya makocha watatu na dakitali mmoja.
Wachezaji na makocha waliopo kambini ni:-
1.       John Christian             49KG l/fly
2.       Abdalah Kassim          52 kg fly
3.       Emillian Patrick          56 kg bantam
4.       Denis Martin                60 kg l/weight
5.       Victor Njaiti                64 kg l/welter
6.       Seleman kidunda         69 kg welter
7.       Mohamed chibumbui   69 kg welter
8.       Mhina Moris                 81 kg l/heavy
9.       Haruna Swanga          91kg   heavy
10.   maximillan Patrick        91+  super heavy
11.   Edward Emanuel          kocha
12.   David Yombayomba      kocha
13.   Remy Ngabo                  kocha
14.   Joseph Magesa              daktari
Wote mnakaribishwa kushuhudia tukio hilo kwa maendeleo ya mchezo wa ngumi

Makore Mashaga
Katibu Mkuu

No comments:

Post a Comment