Tangazo

Pages

Saturday, September 7, 2013

WAJUE MABINGWA WA DUNIA WA UZITO WA KATI (SUPER MIDDLEWEIGHT) WA VYAMA / MASHIRIKISHO MBALIMBALI


Waziri Mkuu Mh,Mizengo Pinda katikati akiwa na mabondia Fransic Miyeyusho kushoto na Fransic Cheka wakati walipo tembelea bungeni Dodoma kwa ajili ya kutambua mchango wao na kuwapongeza picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


IBF AFRICA



to onesmongowi, ONESMO, bcc: me
   
Translate message
Turn off for: Swahili
Na Onesmo Ngowi
Rais wa IBF Africa, Ghuba ya Uarabu na Uajemi na mashariuki ya Kati
 
 
Hivi karibuni Mtanzania Francis Cheka ambaye alikuwa  bingwa wa IBF katika bara la Afrika uzito wa kati (Super Middleweight) alimshinda bondia kutoka Marekani Phil William na kutawazwa kuwa bingwa wa dunia anayetambuliwa na Shirikisho la Ngumi la Dunia (WBF). Ushindi wa Cheka sio tu kwa Tanzania bali na kwa bara la Afrika na dunia yote kwa ujumla.

 

 
Cheka ameungana na mabingwa wengine wa dunia wa uziro wa kati (Super Middleweight) wanaotambuliwa na vyama na mashirikisho kadhaa kama ifuatavyo:
 
 
IBF    -  Carl Froch kutoka nchini Uingereza

WBC -  Andre Ward kutoka nchini Marekani
WBA -  Andre Ward kutoka nchini Marekani
WBO -  Robert Stieglitz kutoka nchini Ujerumani
WBF -   Francis Cheka kutoka nchini Tanzania
IBO   -  Thomas Oosthuizen kutoka nchini Afrika ya Kusini
 
 
Kwa uchache hao ni mabingwa wa uzito wa uzito wa kati (Super Middleweight ) wanaotambuliwa na vyama/mashirikisho hayo niliyoyataja hapo juu. Kati ya mabingwa wa dunia wa mashirikisho/vyama sita vikubwa duniani Afrika imetoa mabindia wawili tu nao ni Francis Cheka kutoka nchini Tanzania na Thomas Oosthuizen kutoka nchini Afrika ya Kusini.

 

 
Ubingwa alioupata Francis Cheka ni wa dunia na hautakiwi upingwe na mtu yeyote yule nje ya ulingo bali wanaotaka kumpinga na kuukebehi wanatakiwa wapande naye ulingoni au wamtafutie mtu wao apande naye ulingino ili apigane na Francis Cheka.

 

 
Kwa bahati mbaya, taratibu na sheria za mchezo wa ngumi haziruhusu mtu yeyote ambaye hayuko kwenye viwango vya ubora wa ngumi agombee ubingwa wa aina yeyote ule.
 
 
Mashirikisho au vyama vya ngumi vimeweka utaratibu maalum wa mabondia watakaoweza kugombea ubingwa wa dunia na mara nyingi ni wale tu walio kwenye viwango vya juu kuanzia namba moja hadi namba tano.

No comments:

Post a Comment