Tangazo

Pages

Monday, September 23, 2013

HAYE APASUKA JICHO, ASHINDWA KUMVAA TYSON



BINGWA wa zamani wa uzito wa juu, David Haye amelazimika kusogeza mbele mpambano wake na Tyson Fury uliopangwa kucheza Septemba 28, ambao ulitakiwa kufanyika jijini Manchester kutokana na kupasuka juu ya jicho lake la kushoto.
Haye ambaye alipoteza mkanda wake wa WBA Julai 2011 kwa bingwa Vladimir Klitschko wa Ukrain, alipasuka Ijumaa alipokuwa anafanya mazoezi na Mcroatia, Filip Hrgovic na kulazimika kushonwa nyuzi sita.
Promota wa Haye amesema katia taarifa yake kuwa kutokana na kushonwa nyuzi hizo ambazo zitatolewa baada ya siku saba ndipo watajua lini anaweza kupanda ulingoni kwa ajili ya pambano hilo, hadi sasa hakuna tarehe iliyopangwa.
"Pamoja na maandalizi kuwa yanakwenda vizuri," alisema Haye mwenye miaka 32. "Nilijiandaa vizuri sana na mambo yalikuwa yanakwenda sawa. Lakini kwa sasa, natakiwa kukabiliana na hali iliyotokea."

No comments:

Post a Comment