Tangazo

Pages

Wednesday, September 4, 2013

CESAR CHAVEZ UMASIKINI ULIMFANYA AJITUMBUKIZE KWENYE MASUMBWI



MEXICO CITY, Mexico
"NLIKUWA  nikimuangalia mama yangu akifua na kupiga pasi nguo za watu  na nilimuahidi siku moja nitampa nyumba na kamwe hatafanya kazi hiyo tena".

Kauli hii siyo yangu mimi, bali ni ya bondia, Julio Cesar Chavez, wakati akisikitishwa  na hali ya umaskini iliyokuwa nayo familia yao hadi akaamua kujikita kwenye mchezo wa masumbwi ili kuiokoa familia hiyo.

Kwa mujibu wa historia ya bondia huyo, alizaliwa Julai 12, 1962 katika kitongoji cha Ciudad Obregon Sonora nchini  Mexico na baba yake,  Rodolfo Chavez, alikuwa mfanyakazi wa reli.
Katika makuzi yake alikuwa akishinda kwenye treni akiwa na dada zake watano na kaka zake wanne.
Chávez anatajwa kuzaliwa kwenye familia maskini  lakini ngumi zikamtoa na kumpa heshima kubwa.

Bondia huyo alianza ngumi za ridhaa akiwa  na umri wa miaka 16 na baadaye akahamia mjini Culiacan ili kuendeleza kibarua chake.

Inaelezwa kuwa kama   kuna mabondia ambao rekodi zao zinajieleza, miongoni mwao ni Chavez.
Rekodi hiyo ni kutokana na kwamba  Chavez aliwahi kusimama ulingoni kwa miaka 10 bila kupigwa na bondia  yeyote.
Katika rekodi hiyo, bondia huyo alipigana mapambano 116, ambapo kati ya hayo alishinda 108 na kati ya hayo 87 alishindwa kwa KO akapigwa 6 na kutoka sare mawili.

Kutokana na umahiri wake, bondia huyo anafahamika kuwa kati ya mabondia ambao walipigana mapambano makubwa  yaliyomfanya kupewa heshima ya bondia bora nchini Mexico.

Kwa mujibu  wa historia ya bondia huyo ambaye alijikita kwenye  ngumi za kulipwa mwaka 1980  kabla ya kutundika gloves mwaka 2005, amewahi kutwaa ubingwa mara sita katika uzani tatu tofauti.

Mbali na sifa hizo, mbabe huyo wa masumbwi vilevile kwenye rekodi yake ana rekodi ya kupigana mapambano  88-0 kabla ya kupoteza moja dhidi ya  Frankie Randall, lakini baadaye akalipiza kisasi mara mbili.

Inaelezwa  kuwa kabla ya pambano hilo alikuwa ameshatoka sare dhidi ya Pernell Whitaker, pambano ambalo alionekana ilikuwa ashindwe.

Mabondia wengine ambao waliwahi kuonja kichapo kutoka kwa Chavez ni  Roger Mayweather, Hector Camacho, Sammy Fuentes.

Hata hivyo pamoja na kustaafu mchezo huo, jina  Chavez bado linatamba kwenye ulingo wa mchezo huo kupitia kwa mwanaye, Julio Chavez, Jr.

Chávez alipigana pambano lake la kwanza la ngumi za kulipwa akiwa  na umri wa miaka  17 na katika pambano lake la 12 lilikuwa ni Machi  4, 1980,ambapo alikutana na Miguel Ruiz,  pambano ambalo lilifanyika mjini Culiacan, Sinaloa.
Katika pambano hilo ikiwa mwishoni mwa raundi ya kwanza, Chavez aliachia konde lililomuangusha Ruiz.

Baada ya pambano hilo bondia huyo aliendelea kushika kasi kwa kuwachapa mabondia kadhaa kabla ya Septemba 13,1984, kutwaa ubingwa wa Feather kwa kumchapa Mmexico mwenzake, Mario Azabache Martinez, katika pambano lililofanyika kwenye ukumbi wa Grand Olympic Auditorium, uliopo mjini Los Angeles, California.

No comments:

Post a Comment