Tangazo

Pages

Thursday, February 28, 2013

MNAMIBIA KUUMANA NA MGHANA UBINGWA WA IBF.


  Albinus (kushoto) akifanya vitu vyake
 Thursday, February 28, 2013 - Dar-Es-Salaam, TANZANIA- Siku kubwa na yenye matumaini mapya katika maisha ya bondia wa Namibai Albinus Felesianu (9(4)-2(1)-0) itawadia hivi karibuni wakati atakapokutana na bodia Herbert Quartey (10(7)-8(6)-0) wa Ghana kugombea ubingwa wa IBF wa dunai uzito wa Unyoya (Featherweight). Albinus alipata mshtuko mkubwa sana na kushangzwa na habari za hivi karubunI kuwa IBF imempa nafasi ya kugombea ubingwa wa dunia wa vijana jambo lililomfanya apate furaha ya ajabu. Albinus Felesianu Albinus (kushoto) akifanya vitu vyake Mtu pekee atakayeweza kuzima furaha yake na kumfanya asiweze kufikia malengo yake katika ngumi ni bondia Herbert Quartey kutoka Ghana ambaye ni moja kati ya mabondia wenye ujuzi mubwa wa kupigana ulingonI. Kama inavyosemwa kuwa "mtoto mtukutu aliyepotea kwenye ngumi anapoomba kurudi kundini na kukaa kufuata kanuni na shaeia za ngumi mchezo wa ngumi humpokea kwa shangwe na nderemo na kumpa mawaidha na ushauri wa kumwendeleza" ndivyo hivyo hivyo Albinus Felesianu na Herbert Quartey watakavyopokelewa na ngumi baada ya pambano lao la tarehe 29 Machi jijini Windhoek, Namibia. Bondia Albinus Felesianu yuko chini ya promosheni ya Kinda Nangolo ambaye anamiliki kampuni tanzu ya Kinda Boxing Promotion na ni promota anayeinukia kwa kasi sana katika tasnia ya ngumi nchini Namibia na barani Afrika

No comments:

Post a Comment