Tangazo

Pages

Wednesday, September 17, 2014

BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' AOMBA SAPOTI YA KUANDALIWA MECHI YA KUTETEA MKANDA WAKE WA WPBF AFRICA




Na Mwandishi Wetu BONDIA Ibrahimu Class 'King Class Mawe' won 11 (KO 4) + lost 1 (KO 0) + drawn 0 = 12  anaeshikilia mkanda wa WPBF Africa katika uzito wa light welterweight amejitokeza hadharani na kusema kwamba mchezo wa ngumi nchini Tanzania aulipi kutokana na malipo yake ni madogo bondia huyo aliyefanikuwa kuwa bingwa baada ya kumpiga Mwansa Kabinga
 mpambano ulio fanyika  june 8 mwaka huu huko  Arthur Davies Stadium, Kitwe, Zambia na kuibuka mshindi katika raundi ya tisa bondia huyo mwenye ndoto ya kuwa bingwa wa dunia katika miaka ya hivi karibuni



 amesema mabondia wa hapa nchini bado awajajielewa kutokana na kuto kuwepo na wafadhili wa kutosha katika mchezo wa masumbwi ila ufadhili mwingi unapelekwa katika mambo ya soka uku wakiuwacha mchezo wa masumbwi auna mwelekeo na sapoti yoyote bondia huyo alijitamba  kwa kujinasibu kuwa kwa hapa nchini akuna bondia ambaye anaweza kumbabaisha katika kipindi hiki kwani yeye kwa sasa yupo matawi ya juu bondia huyo anaefanya mazoezi katika kambi ya Ilala ananolewa na jopo la makocha likiongozwa na Habibu Kinyogoli 'Masta' kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'

 ameomba watu mbalimbali kujitokeza kumsaidia ili atetee mkata wake wa WPBF Africa alioupata Zambia ili awadhilishie watu kuwa uwezo alionao ni mkubwa sana katika masumbwi kingine ni wadhamini wajitokeze kumpa sapoti kwani ana uwezo wa kuwatangazia biashara mbalimbali ukizingatia yeye ni bingwa na bado kijana mdogo mwenye nia ya kufika mbali katika mchezo wa masumbwi nchini

No comments:

Post a Comment