Tangazo

Pages

Friday, March 16, 2012

BOXING REFEREE'S

Referee’s wetu wa Boxing 90% wengi wao sio competent to be a boxing referee, ufahamu wao ni mdogo mno ktk maswala ya boxing, wengi wanafanyia uzoefu kwa kuwa waliwai kucheza ngumi hapo nyuma, ila hawajawai kupata proper training yeyote ya boxing referee.
APPEARANCE:
Wengi wanavaa uniform hazipo smart, shart alijapigwa pasi, viatu hata kiwi awapigi, suruali ndio usiseme.
PST – uniform zao ni trouser black na shati white na necktie red
TPBO – trouser black, shati dark blue, tai black
TPBC – wanavaa kama PST isipokuwa tai zao ni black
KBF – Chama cha Habibu Kinyogoli, wao wanakodi marefa
Referee’s hawa kama nilivyoeleza appearance zao zinatia aibu, hata mgeni wa kheshima akija ni aibu tupu kwa kweli, Ally Bakari a.k.a Champion kama anavyojiita, yeye huwa anavaa suruari njiwa, chini kapiga rubber, shati chafu hataa pasi alijapigwa, umeona wapi suruari ikavaliwa na raba, waangalie marefa wa Intanationa fight wanavyo vaa na kupendeza.
DDC Kariakoo, Francis Miyeyusho na boxer mmoja kutoka Kenya, sanction by  TPBO, Yasin Abdallah Ustaz alimfukuza kwenye ring Antony Luta hasi officiate fight kwa kuwa hakuwa smart na akuvaa uniform za referee za TPBO, hapo nilimpongeza na inatakiwa hivyo awe na msimamo, uwo ni mfano mmoja tu hipo mingi.
REFEREE IN THE RING:
Referee anatakiwa kabla boxer awajapanda kwenye ring yeye refa aende dressing room akawakague na kuwapa maelekezo na sheria zitakazotumika, na kabla awajavaa gloves akague ndipo wazivae. alafu azi sign kwa sheria sasa, Maana glove zinavaliwa dressing room, zamani wanavaa kwenye ring, hili kwetu alipo na alifanyiki na hawajui na hawafahamu.
Boxers wanapopanda kwenye ring, baada ya taratibu zote kufanyika, kama national anthem kupigwa, na Ring announcer ‘ MC ‘ kutangaza kila kitu ndipo Refa anawaita boxers ktkt kuwapa maelekezo ya mwisho kabla fight aijaanza, na kuwakagua kama gumsheed wamevaa, protectors, groves kama zimefungwa vizuri na huwa anawaambia mengi tumezungumza kwenye dressing room, I want clean fight at all time, protect yourself at all time, watch you head at all time, Ukipiga punch chini ya belt hiyo ni low blow ukiludia nakata point, ktkt ya mkanda its ok, above belt it’s ok, when I say stop, unatakiwa kustop na usipige ngumi, break una break faster, touch gloves, boxers wana touch gloves wanaenda neutral corner ready for fight.
Referee wetu awajui haya wanaojua ni wachache sana ntawataja wanaojua wakati nafanya majumuisho yangu, wanaita boxer ktkt wanayowaambia madudu matupu,
Mfano mmoja, Antony Luta, Dimond Jubelee main card Mbwana Matumla vs Francis Miyeyusho, refa Luta alianza kuwaambia boxers sheria za 10 points system wakati wa score cards, kuwa mtu anaweza kuongoza ktk round 7 za awali ila akaja kupigwa round zilizpbaki pake mshindi atakuwa aliongoza mwanzo, alichemka vibaya sana mpaka watu wakaanza kumzomea, akupaswa awaambie hayo japokuwa alikuwa sawa, yaliyopaswa kuzungumziwa pale niliyoyaeleza hapo juu.
DURING THE FIGHT.
Kosa lingine wanalolifanya hawa marefa wetu wa sasa wakati fight inaendelea ikatokea boxer mmoja kapigwa punch kakaa chini, sheria unatakiwa umuhesabia one to eight awe amesimama, na kabla ujamuhesabia unatakiwa uwakikishe the other boxer yupo ktk Neutral corner ndipo uanze kuhesabu, na ikifika nane u make sure boxer keshasimama unatakiwa huu walk back hatua 3 then unamuita boxer akufuate, coming!!!, coming!!! Atakapokuja unamwambia are you ok! Alafu afute glove unamluhusu aendelee na fight,
Refa wetu haya awayafuati tumeshuudia mala nyingi boxer anahesabiwa wakati Yule mwingine ajaenda Neutral corner ilo ni kosa, huwezi kuhesabu wakati the other boxer ajasimama neutral corner, alafu wanahesabu mpaka 10 boxer ajasimama,
Mfano hai mmoja ni refa Emanuel Mlundwa, Dimond Jubelee, Juma Fund vs Fadhili Magia, Juma Fund kapigwa punch kali kaka chini, kahesabiwa mpaka 10, apart from 8, na Mlundwa aku walk back hatua 3 na wala akumuita Juma fundi afute, badala yake akawa anaongea nae mpaka kengere ikagongwa, kama mimi ningekuwa refa wa ile fight ile ilikuwa ni clean KO!
DROP OF GUMSHEED.
Kizuia meno kikianguka marefa wetu huwa wanaokota wenyewe kwa mikono yao ambayo hata gloves hawajavaa, wanamuwekea boxer mdomoni, hii ni hatari kwa afya ya refa na boxer mwenyewe, kizuia meno kile kinakuwa kimelowa damu, mate, na kimeanguka chini kwenye sakafu chafu watu wamekanyagakanyaga,
Unatakiwa kikidondoka usimamishe fight, huu make sure umevaa surgical glove’s mikononi, hiokote, ipeleke ktk corner ya boxer muhusika, trainer na 2nd wake wataisafisha na wao ndio wanaposwa kumvalisha boxer wao, kosa hili linafanyika karibu kila fight. Surgical gloves box moja la 100pcs wanuza elfu 6 tu rakini marefa wetu wanapanda ulingoni wakiwa awajavaa glove’s. alafu wanashika kwa mikono wanamuwekea boxer mdomoni ni hatari kwa afya yake,

CURRENT REFEREE’S
Omary Yazidu, Said Chaku, Abdallah Mpemba, Ally Bakari “Champion”, Antony Luta, Issa Makaranga, Ramson Basta, Kondo Nassoro, Pembe Ndava, Emanuel Mlundwa, Names Kavishe, Mark Hatia, Yasin Abdallah Ustaz, John Chagu na Lucas Msomba.
Hawo ambao nime wa bold ndio competent referee’s wa ukweli, International referee’s, wengi wao awaonekani sana siku hizi mpaka big fight or special event or special case peke yake.
Swala hao waliobaki nani kawapa urefa??????????????????????
Wamekuwa trained na nani????? Mkufunzi gani kutoka vyama vya ngumi vikubwa duniani aliekuja kuwa train hawa marefa wetu??
Serekali na BMT mnajua haya?? Kuwa hawa marefa sio competent, hawana hata certificate zinazowatambulisha kuwa ni profesionaer boxing referee’s
Ustaz Yasin Abdallah – President wa TPBO huko Tanga ktk fight zake alikuwa refa na Judge nani kampa kibali cha yeye kuwa refa??
Tunacheza na maisha ya watu, akifa mtu sasa hivi kwenye ring tunawafungulia kesi ya mauwaji. Ally Bakari “ champion “, Said Chaku wamekuwa trained na nani????
Huko nyuma tumeshuhudia boxers wakifa ulingoni kama Mandera Rajabu, Antony Ndaki na wengineo, sheria na watu walikuwa wamelala ila safari hii mtu akifa kwenye ring tunawashtaki, marefa, Judge’s, chama kilichotoa kibali na tuna appoint the best Lawyer in town. Refa yeyote atakae panda ulingoni kama hana certificate inayo mcertify kuwa ni boxing referee ajiandae.
Naomba kuwakilisha
Mdau.

No comments:

Post a Comment