Tangazo

Pages

Thursday, May 24, 2012

WATANZANIA WATAKIWA KUWEKEZA KWENYE NGUMI



Kwakuwa Tanzania imetoa Rais Shirikisho la Ngumi la Kimataifa katika bara laAfrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi, ni muhimu Watanzania mmoja mmoja,taasisi na makampuni wakajua fursa zilizopo kwenye medani ya ngumi za kulipwa.



Mchezowa ngumi za kulipwa ni mchezo pekee unaoweza kumpa mtu, taasisi au kampuni inayowekezafaida kubwa kwa kipindi kifupi sana. Ni mchezo ambao mbali na mingine ambayohuwa inategemea uchezaji wa ushirikiano wa wale wanaoshiriki una hamasa kubwasana hivyo kutoa fursa kubwa kuupromoti au kuudhamini.


Katikakipindi changu cha uongozi wa bara la Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba yaUajemi nitajitahidi sana ili mtanzania mmoja mmoja, taasisi pamoja namakampuni ya biashara yaweze kufaidika sana katika mchezo huu.

Watuwengi huwa na imani hasi kuhusu mchezo wa ngumi na hivyo kutoweza kujua thamanina faida zinazopatikana kwenye mchezo huu.

Mbalina kutoa ajira kwa njia ya kipato wanazopata washiriki kwa maana ya mabondia, kunapia ajira kwa wale wanaohudumia hatua kwa hatua wakati wa maandalizi ya pambanokama vile makampuni ya matangazo kama vile magazeti, redio, televisheni na blogs mbalimbali.

Aidha makampuni za huduma kama vile vinywaji, na vyakula. Makampuniya nguo. Kamapuni ya huduma kama vile mapambo. Makampuni yanayotoa huduma ya utalii na usafiri. Makampuni ya huduma za ulinzi, Pia, makampuni ya bima yanawezasana kutoa huduma kwa washiriki pamoja na mapromota wa mchezo huu.

Watanzaniahatuna budi kuchangamkia fursa hizi zinazotolewa na mchezo huu unaopendwa sana ulimwenguni. Mchezo huu mbali na soka ndio mchezo unaoweza kuingiza pesa nyingisana kwa waandaaji, mabondia na wale wote wanaoshiriki. Wenzetu kama Afrika yaKusini, Ghana, Namibia, Zambia wako mbali sana kwa uwekezaji huu.

Napendakuwahimiza watanzania watumie nafasi hii nzuri kujifunza na kuwekeza kwenyemchezo huu. Shirikisho la Ngumi la Kimataifa IBF chini ya uongozi wangu litakuwalinatoa semina mbalimbali kwa wadau wa mchezo huu ili waweze kujua fursa zilizokona kuzitumia barabara!

Nafasiyangu itaniwezesha kuipendelea Tanzania kwa kiwango kikubwa kwani “mtu ni kwao” hivyo nadhamiria kuitumiafursa hii barabara!

Nitakuwana ofisi za aina tatu. Moja nitakuwa na ofisi kwenye Shirikisho hili kule NewJersey, Marekani kama kitengo kinachohudumia mabara (continents). Nitakuwa naofisi nyingine kwenye nchi za Mashariki ya Kati (Middle East) na Ghuba yaUajemi (Persian Gulf) kule Dubai, United Arab Emirates (UAE).

Aidhanitakuwa na ofisi za shirikisho hili hapa kwetu Dar-Es-Salaam, Tanzania kuhudumianchi za bara la Afrika (Africa continent).

Ninaondokakwenda kwenye mkutano mkuu wa mwaka kule Honolulu, Hawaii, Marekani nikiwanimejiandaa vyema kuiwakilisha Tanzania. Tayari tumeshapata miadi ya kukutanana balozi mbalimbali katika nchi za Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba yaUajemi (ubalozi wa Tanzania jijini Washington DC ukiwa mojawapo) ya kuzungumzianamna gani tutakavyoweza kushirikiana na serikali zao kukuza “Sports Tourism” programambayo nina furaha kubwa kuianzisha ndani ya IBF/USBA.

Karibunitushirikiane kuendelza mchezo wa ngumi.

Imetolewana:
OnesmoNgowi
Rais wa Shirikisho laNgumi la Kimataifa na Chama Cha Ngumi Cha Marekani (IBF/USBA)
Katika bara la Afrika,Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi

No comments:

Post a Comment