Tangazo

Pages

Wednesday, May 2, 2012

PAMBANO LA NGUMI - VIJANA HALL,KINONDONI


BigRight PROMOTION ikishirikiana na T, ASENGA investment imeandaa pambano la ubingwa wa taifa kati ya RAMADHAN KUMBELE  na JAMES MOKIWA.

Pambano hili litakuwa katika uzani wa Bantam weight la raundi kumi. 

Chini ya usimamizi wa Tanzania Profesional Boxing Organization (T.P.B.O) litakalofanyika  Mei  20/2012 siku ya jumapili katika Ukumbi wa Vijana, uliopo Kinondoni.

Katika ubingwa huo pia kutakuwepo na mapambano mengi ya utangulizi na yenye upinzani wa hali ya juu.

Kama pambano la Heavyweight ANORD "biggie"YOHANA 125kg, atapambana na KARIM 'big paquiao"SALUM 120kg, pambano la raundi 8. 

Mapambano mengine ni feather weight-kati ya , Doi Miyeyusho, ambaye  atacheza na Jumanne Mtengela, pambano la raundi 6, lightweight-Jafar Majia na Daudi Muhunzi, raunda 6, Middle weight-Franci Suba na Joseph Peter'  raundi 6. .

Mapambano mengine , Fly weight, Sadat Miyeyusho atacheza na Swedi Hassan, Martin Richard na Yohana Thobias , Amos Mwamakula na Mwaite Juma,  hawa watacheza raundi nne nne.

Aidha katika mapambano hayo kutakuwa na show za boxing za watoto kwa ajili ya kuhamasisha na kukuza vipaji. 

Pia katika mpambano huo kutakuwawepo na projector itakayoonesha mapambano ya FRANCIS MIYEYUSHO NA MBWANA MATUMLA i,ii,& iii.na mapambano mengine ya Francis Cheka pia yataoneshwa ukumbini hapo.

No comments:

Post a Comment