Tangazo

Pages

Wednesday, September 17, 2014

BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' AOMBA SAPOTI YA KUANDALIWA MECHI YA KUTETEA MKANDA WAKE WA WPBF AFRICA




Na Mwandishi Wetu BONDIA Ibrahimu Class 'King Class Mawe' won 11 (KO 4) + lost 1 (KO 0) + drawn 0 = 12  anaeshikilia mkanda wa WPBF Africa katika uzito wa light welterweight amejitokeza hadharani na kusema kwamba mchezo wa ngumi nchini Tanzania aulipi kutokana na malipo yake ni madogo bondia huyo aliyefanikuwa kuwa bingwa baada ya kumpiga Mwansa Kabinga
 mpambano ulio fanyika  june 8 mwaka huu huko  Arthur Davies Stadium, Kitwe, Zambia na kuibuka mshindi katika raundi ya tisa bondia huyo mwenye ndoto ya kuwa bingwa wa dunia katika miaka ya hivi karibuni



 amesema mabondia wa hapa nchini bado awajajielewa kutokana na kuto kuwepo na wafadhili wa kutosha katika mchezo wa masumbwi ila ufadhili mwingi unapelekwa katika mambo ya soka uku wakiuwacha mchezo wa masumbwi auna mwelekeo na sapoti yoyote bondia huyo alijitamba  kwa kujinasibu kuwa kwa hapa nchini akuna bondia ambaye anaweza kumbabaisha katika kipindi hiki kwani yeye kwa sasa yupo matawi ya juu bondia huyo anaefanya mazoezi katika kambi ya Ilala ananolewa na jopo la makocha likiongozwa na Habibu Kinyogoli 'Masta' kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D'

 ameomba watu mbalimbali kujitokeza kumsaidia ili atetee mkata wake wa WPBF Africa alioupata Zambia ili awadhilishie watu kuwa uwezo alionao ni mkubwa sana katika masumbwi kingine ni wadhamini wajitokeze kumpa sapoti kwani ana uwezo wa kuwatangazia biashara mbalimbali ukizingatia yeye ni bingwa na bado kijana mdogo mwenye nia ya kufika mbali katika mchezo wa masumbwi nchini

Monday, September 15, 2014

DVD MPYA KUTOKA SUPER D BOXING COACH AND PROMOTION MAYEATHER VS MAIDANA 2





WBA/WBC welterweight champion Floyd Mayweather Jr (47-0, 27 KOs)
win by
Pointi 115-112, 116-111, 116-111.
 Marcos Maidana
(35-5, 31 KOs)
SASA ZINAPATIKANA KWA WEPESI ZAIDI KUTOKA SUPER D BOXING COACH AND PROMOTION MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI KARIAKOO  PIGA SIMU 0754/0787/0713-406938
 DVD YA MABONDIA MOHAMED MATUMLA VS NASSIBU RAMADHANI LILILOFANYIA  DESEMBA 25/ 2013 SASA ZIPO MTAANI KUTOKA SUPER D BOXING COACH AND PROMOTION MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI KARIAKOO  PIGA SIMU 0754/0787/0713-406938
DVD MPYA YA BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' VS
Mwansa Kabinga WA ZAMBIA
 08-06-2014
LILILOFANYIKA
Arthur Davies Stadium, Kitwe, Zambia NA
KURUDI NA UBINGWA WA WPBF AFRICA  SASA ZINAPATIKANA SUPER D BOXING COACH AND PROMOTION MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI KARIAKOO  PIGA SIMU 0754/0787/0713-406938

Mashindano ya ngumi ya wavuvi Boxing Tournament 13/09/2014


Taarifa kwa vyombo vya habari
     Yah:- Mashindano ya ngumi ya wavuvi Boxing Tournament 13/09/2014
                                         Bagamoyo.
Shirikisho la ngumi Tanzania (BFT) limeaandaa mashindano ya ngumi ya wavuvi Boxing TOUNAMENT yatakayoanza kufanyika tarehe 13/09/2014 katika fukwe za Bagamoyo na baadaye kuendelea katika fukwe mbalimbali.
Lengo la mashindano hayo ni  kuhamasisha jamii ya wavuvi na watu wanaowazunguka kujishughurisha na masuala ya michezo na hasa mchezo wa ngumi baada ya shughuri zao za uvuvi na kuwafanya kuondokana na vitendo viovu vinavyotokana na utumiaji wa vilevi mbalimbali kupita kiasi na zaidi kuvumbua vipaji kutoka katika jamii hiyo ikiwa pamoja na kuwapa burudani.
Katika utafiti uliofanywa na BFT tumegunduwa kuwa katika jamii ya wavuvi wapo wengine wanaopenda michezo hasa mchezo wa ngumi hii ni kutokana na asili ya kazi yao ya uvuvi ya kutumia nguvu za mikono kwa ajili ya uvuvi na akili nyingi hivyo tumeazimia kuanza kuwafikia kwa vitendo kwa kufanya mashindano katika maeneo yao ili kuwahamasisha kijiingiza zaidi katika michezo.
Mashindano hayo yatakuwa yanafanyika kila siku ya jumamosi kwa fukwe mbalimbali za  bahari ya hindi na baadaye kuhamia katika fukwe za maziwa makuu.
Mashindano haya yamedhaminiwa na kampuni ya Sam & Anzai Boat Builder C.,Ltd kwa kushirikiana na  C&G
Makore Mashaga
Katibu mkuu.

DVD MPYA KUTOKA SUPER D BOXING COACH AND PROMOTION MAYEATHER VS MAIDANA 2




WBA/WBC welterweight champion Floyd Mayweather Jr (47-0, 27 KOs)
win by
Pointi 115-112, 116-111, 116-111.
 Marcos Maidana
(35-5, 31 KOs)
SASA ZINAPATIKANA KWA WEPESI ZAIDI KUTOKA SUPER D BOXING COACH AND PROMOTION MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI KARIAKOO  PIGA SIMU 0754/0787/0713-406938
 DVD YA MABONDIA MOHAMED MATUMLA VS NASSIBU RAMADHANI LILILOFANYIA  DESEMBA 25/ 2013 SASA ZIPO MTAANI KUTOKA SUPER D BOXING COACH AND PROMOTION MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI KARIAKOO  PIGA SIMU 0754/0787/0713-406938
DVD MPYA YA BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' VS
Mwansa Kabinga WA ZAMBIA
 08-06-2014
LILILOFANYIKA
Arthur Davies Stadium, Kitwe, Zambia NA
KURUDI NA UBINGWA WA WPBF AFRICA  SASA ZINAPATIKANA SUPER D BOXING COACH AND PROMOTION MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI KARIAKOO  PIGA SIMU 0754/0787/0713-406938

TASWIRA ZA MAPAMBANO MAWILI YA NGUMI MKOANI KILIMANJARO





Mapambano ya utangulizi yakaanza .
Mgeni rasmi katika mapambano mawili ya ngumi ya kimataifa ,mkuu wa wilaya ya Hai ,Novatus Makunga akizungumza wakati wa mapambano hayo kati ya Bondia Said Yazidu(Tanzania) na Djamel Dahou(Aljeria) .
Muandaaji wa Pambano hilo,Andrew George akionesha mkanda wa Ubingwa wa Afrika ulikuwa ukigombewa na Bondia Alibaba Ramadhan(Tanzania) na Aleck Mwenda(Malawi).
Mgeni rasmi ,Novatus Makunga akonesha mkanda huo kwa mashabiki.
Pambano likaanza kati ya Bondia,Alibaba(Mwenye Bukta nyekundu) na Aleck Mwenda(Mwenye Bukta nyeusi)
Alibaba akajaribu kupiga ngumi kadri alivyoweza.
Aleck Mwenda pia akajibu mapigo ingawaje yake yalionekana makali zaidi.
Bondia Mwenda alikuwa mzuri sana katika kujikinga.
Mwenda akamsukumia Alibaba ngumi za kutosha.
Alibaba akaenda chini mara kadhaa lakini alinyanyuka.
Round 10 zikamalizika uamuzi wa majaji ukingojewa. huku dalili zikionesha dhahiri ,Aleck Mwenda atakuwa ameshinda.
Akiwa amebebwa na wamalawi wenzake na kushangilia ,hakuamini alichosikia masikioni mwake baada ya mshindi kutangazwa Alibaba.
Furaha ikahamia kwa Alibaba.
Mashabiki wakaingia ulingoni kwa Bondia na Chupa za Bia.
Kamanda wa Polisi wa wilaya OCD, Deodatus Kasindo akamkabidhi mkanda Alibaba.
Alibaba akifurahia mkanda wake wa Kwanza baada ya kutangazwa Bingwa wa  Ngumi Afrika. 
Furaha ya Ushindi.
Likafuatia Pambano la Ubingwa wa Dunia Kati ya Bondia ,Djamel Dahou(Aljeria) na Said Yazidu .
Bondia Said Yazidu wa Tanzania akapanda ulingoni.
Mpambano ukaanza.
Kila mmoja akamvizia mwenzake.
Bondia Yazidu akapigwa vitasa kadhaa.
Akakaaa kwa mara ya kwanza.
Akasimama kisha akajitutumua ,akapigwa kitasa tena ,
Akakaa kwa mara nyingine.
Akasimama tena akachezea ngumi za kutosha .
Zikampeleka chini kwa mara ya tatu.
Akanyanyuka kwa Mbinde .
Ikashindikana na Bondia ,Dahou akashinda kwa KO ndani ya dakika 2 na sekunde 7 katika round ya kwanza.
Dahou akatangazwa Bingwa.
Mgeni rasmi ,mkuu wa wilaya ya Hai,Makunga akamkabidhi mkanda ,Bondia Dahou.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya jamii kanda ya kaskazini.

Saturday, September 13, 2014

NGUMI ZILIVYOPIGWA MOSHI SIKU YA IJUMAA

Bondia Elick Mwenda kushoto wa Malawi akikwepa ngumi  wakati wa mpambano wake na bondia Allybaba Ramadhani   uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Allybaba alishinda kwa pointi mpambano huo Picha na SUPERD BLOG
Bondia Raymond Mbwago kushoto akipambana na Iddi Pialali wakati wa mpambano wao uliofanyika Moshi katika ukumbi wa YMCA Hall Pialali alishinda kwa K,O ya raundi ya Nne picha na SUPERD BLOG
Allybaba Ramadhani
Bondia Raymond Mbwago kushoto akipambana na Iddi Pialali wakati wa mpambano wao uliofanyika Moshi katika ukumbi wa YMCA Hall Pialali alishinda kwa K,O ya raundi ya Nne picha na SUPERD BLOG
Bondia Shomari Milundi kushoto akipambana na Saimoni Zabron wakati wa mpambano wao uliofanyika Moshi mpambano huo walitoka Droo ya kufungana point picha na SUPERD BLOG

Bondia Said Yazidu kushoto akipigwa ngumi na Djamal Dahou wa Algelia Dahou alishinda kwa K,O ya raundi ya kwanza ya mpambano huo picha na SUPERD BLOG