Tangazo

Pages

Friday, January 1, 2021

SUPER D BOXING PROMOTIOBN KUMRUDISHA HAMISI MAYA ULINGONI APRIL 2

 



NA MWANDISHI WETU

BONDIA HAMISI MAYA sasa kupanda ulingoni rasmi April 2 katika ukumbi wa Sabasaba Hall uliopo katika viwanja vya Sabasaba akimvaa bondia Alvin Omondi wa Kenya mpambano wa Raundi 8 utakaopigwa katika uzito wa KG 66


Akizungumza kuusu mpambano uho Mratibu wa pambano hilo Chaurembo Palasa amesema kuwa baada ya muda mrefu kukaa kimya kwa bondia huyo sasa anaibuliwa upya na kampuni tanzu ya kizarendo ya Super D Boxing Promotion ambao ndio waandaaji wa mpambano uho kwa sasa


Hamisi Maya ambaye ni bingwa wa GBC mkanda unaotambulika Duniani ambapo mpaka sasa anasifika kwa kuwapiga mabondia mbalimbali akiwa nje ya nchi ambapo alishawai kumpiga K,O mbaya sana Jems Onyango wa Kenya mpambano uliofanyika Charter Hall, Nairobi  Kenya na kurudi na ubingwa wa Afrika na kumgalagaza bila ya huruma bondia Piergiulio Ruhe wa ujerumani na kufanikiwa kuruni na mkanda


Alisema Palasa ata hivyo mapromota wengi wamekuwa wakimkwepa Maya kutokana na uchezaji wake awapo ulingoni ni kama bondia aliyekusudia kuuwa mtu akiwa mchezoni ndio mana ajapata mapambano tangu mwaka 2019 hata hivyo kupitia kampuni yetu ya Super D Promotion tunampa nafasi ya kuonesha Kipaji chake kwa mara nyingine kwa mwaka uhu 2021

aliongeza kwa kusema kuwa mbali na mpambano uho pia kutakuwa na mapambano mengine ya lkukata na shoka ambapo bondia machachali awapo ulingoni Vicent Mbilinyi atazipiga na George Onyango na Fransic Miyeyusho atazipiga na Gabriel Chola wakati Hamidu Kwata atazidunda na Jems Kibazange na juma Abdul wataoneshana kazi na Hamza Mchanjo na Bakari Magona atazipiga na Emanuel Mwakyembe



Tuesday, December 15, 2020

SUPER D AMSAINISHA BONDIA HAMISI MAYA KUZIPIGA NA MMISRI FEB 14 SABA SABA HALL

Promota wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akiwa na bondia Hamisi Maya baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga 14 february 2021 katika ukumbi wa Saba saba Hall uliopo katika viwanja vya maonesha Saba saba Maya atacheza na Ahmed Hendy kutoka Egypt

Bondia Hamisi Maya kulia akisaini mkataba wa kuzipiga na Ahmd Hendy kutoka Egpty mpambano utakaofanyika katika ukumbi wa sabasaba hall uliopo katika viwanja vya maonesho ya biashara Saba Saba kushoto ni promota wa mpambano huo Rajabu Mhamila 'Super D' kutoka katika kampuni ya Super D Boxing Promotion

 Promota wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' wa pili kushoto akibadilishana mkataba na bondia Hamisi Maya baada ya usaini mkataba uho kushoto ni kocha wa Maya              Salum Lusasi



Na Mwandishi Wetu


PROMOTA wa mchezo wa masumbwi nchni Rajabu Mhamila 'Super D' amemsainisha bondia Hamisi Maya kwa ajili ya kuzipiga na Ahmed Hendy kutoka Egyty mpambano wa raundi 8 utakaofanyika katika ukumbi wa saba saba hall uliopo katika viwanja vya maonesha vya sabasaba


akizungumza mara baada ya kutiliana saini katika mkataba wa kuzipiga promota Super D amesema kuwa Maya ni bondia bora mchini ambapo mwaka jana alinyakuwa ubingwa wa mabara wa GBC aliounyakuwa nchini Ujerumani


na kufanikiwa kurudi na ubingwa uho hata hivyo mpaka sasa ajautetea hivyo kampuni ya kizalendo ya Super D Boxing Promotion tumeamua sasa kumuinua kwa kumuandalia mpambano wa kimataifa hapa hapa nyumbani ili aoneshe uwezo wake na kipaji alicho nacho

hili apate kukionesha mbele ya jamii bondia huyo bingwa wa Ulaya atazipiga nchini kwake mara ya kwanza baada ya kunyakuwa ubingwa uho


nae Maya ameshukuru kwa kampuni ya Super D Boxing Promotion kumsainisha kwa ajili ya mpambano wake mwingine wa kimataifa utakaofanyika hapa nchini 


hivyo naomba mashabiki wangu waje kwa wingi ili niwaoneshe radha ya mchezo wa masumbwi walio ikosa kwa muda mrefu sasa nitacheza kwa kujivunia kwa kuwa nitakuwa katika uwanja wa nyumbambani alisema Maya


Tuesday, October 27, 2020

SUPER D AMNOWA VICENT MBILINYI KUMKABILI SHEDRACK IGNAS NOVEMBA 28 MASAKI


Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa Masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' akimfundisha bondia Vicent Mbilinyi kupiga ngumi yenye mkunjo wa chini 'UPCAT' kwa ajili ya maandalizi yake na Shedrack Ignas litakalofanyika Novemba 28 katika ukumbi wa Nexrt Door Arena

 Na Mwandishi wetu


BONDIA Vicent Mbilinyi yupo katika maandalizi mazito sana katika kujiandaa kwake kwa mpambano wake na Shedrack Ignas utakaofanyika Novemba 28 katika ukumbi wa Nextri Door Arena Masaki Dar es salaam

akizungumza wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa na pambano hilo Mbilinyi amesema kuwa yeye ngumi ni kazi yake hivyo anaiheshimu kwa kufanya mazoezi kwa bidii na wakati muhafaka kabisa kwani ndio moja na yaisha yake ya kila siku

alivyo ulizwa amejipangaje kumkabili bondia Shedrack Ignas ambaye ni mgumu pia ni nunda kwa uvumilivu wa ngumi hapa nchini

amesema ajakutana na ngumi kali hivyo ajipange kwa kipigo kitakatifu ambacho atampatia bila huruma yani hakika katika ngumi nimejifunza mambo mengi hususani nilivyokwenda safari za nje hivyo siwezi kukubali kupigwa kizembe na kwa uraisi hapa Tanzania

Nae kocha wake ambaye ni kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kwamba ana shaka na bondia wake huyo kwani yupo fiti na mtiifu wa mazoezi hivyo ushindi kwake kama kumsukuma mlevi kwani ngumi ni kipaji nae anacho hivyo anatumia kipaji 


Saturday, October 3, 2020

IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' NA SIMON NGOMA WATAMBULISHA MPAMBANO WAO WA NOVEMBA 27 PTA

Promota Ernest Evarast kutoka kampuni ya Mopao katikati akiwainuwa mikono juu mabondia Simon Ngoma kutoka Zambia kushoto na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' wakati wa kutambulisha mpambano wao wa ubingwa wa Dunia wa GBC utakaofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar es salaam novemba 27

 Mabondia pamoja na makocha wao wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutambulisha mpambano wao wa novemba 27 katika ukumbi wa PTA Sabasaba  kulia bondia Simon Ngoma kocha wake Antoni Mwaba Kocha wa wa kimataifa wa mchezo wa ngumi Tanzania Rajabu Mhamila 'Super D' Bondia Ibrahimu Class King Class Mawe Dkt Hadija Hamisi Promota  Everist Ernes na Ubwa Salumu



NA MWANDISHI WETU

BONDIA Ibrahimu class 'King Class Mawe' amekutanishwa uso kwa uso na mpinzani wake Simon Ngoma kutoka Zambia ambaye alikuja kusaini mkataba wa kuzipiga Novemba 27 katika ukumbi wa PTA Sabasaba

akizungumzia mpambano huo Class amesema kuwa yeye yupo fit ata kwa sasaivi kwa kuwa moto wake bado aujazimika unajua hivi karibuni nimetoka kucheza mchezo na Nassibu Ramadhani na nikafanikiwa kumtwanga bila huruma hivyo na huyu nampiga kama bag naomba watanzania wani sapoti kwa hali na mali na sito wahangusha

ata hivyo naomba wadhamini wajitokeze kwa wingi kwani kwa sasa mchezo wa ngumi unaonekana live katika Luninga na umekuwa kwa kira hidara hivyo wadhamini mjitokeze kupromoti mpambano wa masumbwi nchini usonge mbele

nae Simoni Ngoma kutoka Zambia amesema kuwa kati ya Tanzania na Zambia ni ndugu hila kwa hili udugu utakaa pembeni na nitamtwanga bila huruma Class

nae promota wa mpambano huo Evarist Elnest aliongeza kwa kusema kuwa mbali na mpambano uho kutakuwa na mapambano mengine yenye upinzani zaidi ya hiro ambapo bondia Said Chino atapambana na Haidari Mchanjo na Abdi Kivu atapigana na Maisha Samsoni

ameomba mashabiki kujitokeza kwa wingi ili waujaze ukumbi pia ameomba wadhamini wajitokeze kwa wingi kwani nafasi zipo kwa ajili ya udhamini na mpambano bodo tuna utangaza  nae kocha wa bondia Class Kocha wa Kimataifa  Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa sasa class yupo vizuri na tunaitaji kumbadilisha kidogo katika upiganaji wake ili arete furaha kwa nchi ya Tanzania unajua amebeba watanzania wote watakuwa wanamuangalia Dunia nzima kwa njia mbalimbali hivyo tunategemea ushindi wa mapema alisema Super D

Friday, September 11, 2020

NGUMI KUPIGWA NOVEMBA 28 NEXT DOOR MASAKI

Bondia Imani Daidi Mapambano kushoto akituni shiana misuli na Japhert Kaseba Baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Novemba 28 utakaofanyika katika ukumbi wa Nextri Door Masaki katikati ni mratibu wa mpambano uho Amosi Nkondo 'Amoma'
Bondia Imani Daudi Mapambano kushoto akitunishiana misuli na Japhert Kaseba baada ya kusaini kuzipiga Novemba 28 Dar es salaam
Bondia Swalehe Mkalekwa kushoto na Ramadhani Shauli wakitunishiana misuli baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Novemba 28 katika ukumbi wa Next Door uliopo Masaki Dar es salaam
Mratibu wa mpambano wa masumbwi Amosi Nkondo 'Amoma' katikati akiwainuwa mikono juu mabondia Paul Kamata kushoto na Kanda Kabongo
Bondia Paul Kamata kushoto akitunishiana misuli na Kanda Kabongo baada ya kusaini mkataba 

 

Thursday, July 30, 2020

MABONDIA ABDALLA PAZI NA TWAHA KIDUKU WATAMBULISHA MPAMBANO WAO WA AUGUST 28 UWANJA WA UHURU

Mabondia Abdallah Pazi kushoto na Twaha Kiduku wakiangaliana kwa usongo wakati wa kutambulisha mpambano wao utakaofanyika katika uwanja wa Uhuru August 28 katikati ni Promota wa mpambano uho Jay Msangi 'Jiwe Gumu'

Promota wa mpambano wa masumbwi nchini Jay Msangi 'Jiwe Gumu' katikati akiwatambulisha mabondia Abdallah Pazi kushoto na Twaha Kiduku watakaopambana August 28 katika uwanja wa Uhuru Dar esa Salaam

SUPER D AMNOWA JUMA CHOKI KUJIANDAA KUMKABILI EMANUEL MWAKYEMBE AUGUST 14 MLIMAN CITY


Bondia Juma Choki kushoto askioneshana Umwamba wa kutupiana makonde na bondia wa kimataifa Ibrahimu Class wakati wa mazoezi yake katika Kambi ya Super D Coach Shule ya Uhuru ya kujiandaa na mpambano wake na Emanuel Mwakyembe utakaofanyika Augost 14 Mlimani City Dar Es Salaam



Bondia Vicent Mbilinyi kushoto akipambana na Juma Choki katika mazoezi yaliyofanyika katika Kambi ya Super  D Coach Shule ya Uhuru Dar Esa salaam Choki anajiandaa na mpambano wake na Emanuel Mwakyembe utakaofanyika augost 14 katika ukumbi wa Mlimani City
Na Mwandishi Wetu

Bondia Juma Choki anaye jiandaa na mbambano wake dhidi ya Emanuel Mwakyembe AUgust 14 katika ukumbi waMlimani City jijini Dar es es salaam amejinasibu kumpiga bondia huyo na kuendeleza ubabe baada ya mara ya kwanza kumpiga na kuwa bingwa wa ubingwa wa king of The Ring katika mashindano yaliyofanyika mwaka jana

akijinasibu bondia huyo alivyotembelewa kambini kwake kwa Super D Coach iliyopo shule ya Uhuru Jijini Dar es salaam 

Amesema kuwa mwakembe ana uwezo wa kukanyaga moto wake ata siku moja kwani kichapo alichompa mara ya kwanza kitakuwa zaidi ya kile 
naomba mashabiki waje kuangalia kichapo nitakachompa ulingoni 
 kwani ndipo pa kuoneshana uwezo kama anavyosemaga kocha Super D Kazi Kazi No Pain No Gain yani siku hiyo patachimbika hivyo mwakyembe ajipange sana kwana mazoezi ninayofanya na mbinu ninazofundishwa sio za kitoto hatari tupu

Nae kocha wa bondia huyo Rajabu Mhamila 'Super D' amesema hii ni vita kubwa sana kwa kuwa kocha wa mwakyembe  Edward Lwiyakwipya wamesoma nae pamoja katika ngazi kubwa ya kozi ya kimataifa hata hivyo mimi nina mbinu nyingi zaidi yake ndio mana nilimtwanga katika mpambano wa kwanza na sasa naenda kupiga begi langu tena ata hivyo nita akikisha napata ushindi usiokuwa wa kuwachosha majaji hivyo matumaini yangu ni kumpiga k,o mbaya zaidi

ikumbukwe kuwa mabondia wote wenye viwango vya juu nchini wanatoka kwangu ukiangalia mabondia wote wakubwa wanatoka kwangu
wanakuwa na viwango vya kimataifa hivyo najivunia kwa hilo ukiangalia mabondia wanaotoka kwangu akuna ata mchovyu mmoja alijinasibu Super D

Aliongeza kwa kusema mikono yake wamepita mabondia wengi sana akiwemo Sanday Kiwale, Idd Mkwera Vicent Mbilinyi Ibrahimu Class' King Class Mawe' Shomali Milundi  Shabani Kaoneka na mabondia mbalimbali nchini wote wamepita katika mikono yangu kwa njia moja au nyingine hapa ndio No Pain No Gain kazi kazi hivyo wapenzi wa ngumi muje kwa wingi kuangalia kazi hii ambayo aita muacha mtu salam siku hiyo katika viwanja vyua mlimani City