Tangazo

Pages

Thursday, July 9, 2020

BONDIA HASSANI MWAKINYO ATANGAZA MPAMBANO WAKE WA AGOST 14 MLIMANI CITY ATAMVAA TSHIBANGU KAYEMBE WA DRC YA CONGO

Bondia Hassani Mwakinyo kushoto akizungumza na wahandishi wa habari wakati akitangaza mpambano wake wa Agost 14 utakaofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Dar Esa Salaam Tanzania wa pili ni Mlatibu wa mpambano uho Beatrice Said na kulia ni bondia Tonny Rashidi nae atamsindikiza Mwakinyo siku hiyo Picha na Super D


Mlatibu mkuu wa mapambano Beatrice Said kulia ambaye ameandaa mchezo wa masumbwi yatakayofanyika Agost 14 akiwa na bondia Tonny Rashidi atakae tetea ubingwa wake huo na Gabriel Ochieng wa Kenya  

Mratibu wa mpambano wa masumbwi Beatrice Said akiwa na bondia Hassani Makinyo wakati wa kutangaza mpambano wake wa agost 14 utakaofanyika katika ukumbi wa mlimani city




BONDIA Mtanzania Hassan Mwakinyo anatarajia kupanda ulingoni Agosti 14 mwaka huu kumenyana na Bondia kutoka DRC ya Congo Tshibangu Kayembe.
Pambano hilo la aina yake la kuwania ubingwa wa WBF linatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Mlimani city ambapo mabondia hao watapambana raundi 12.
Akizungunzia mtanange huo Mwakinyo amesema yuko tayari kwa pambano hilo kwani amejiandaa vya kutosha kuhakikisha anamaliza pambano hilo mapema.
Amesema, maandalizi mazuri ambayo ameyafanya na kuendelea kuyafanya yanazidi kumpa morali zaidi kuelekea pambano hilo ambalo hatokubali kuiangusha Nchi.
"Tarehe 14 mwezi ujao natamani sana pambano lifike hata siku zikimbie ziwe tano tano, nimejiandaa na naendelea kujiandaa sina shaka wala hofu na bondia yoyote yule aje tu tukutane ulingoni,"
Aidha Mwakinyo alimuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuri kuunga mkono jitihada za mabondia hapa nchini kama ambavyo amefanya mambo makubwa katika kuendeleza  nchi na jina lake kuzidi kuwa kubwa.
Anasema Rais akisapoti mchezo huo hata wao mabondia itakuwa vyema kwao na itazidi kuwapa morali ya hali ya juu kuzidi kulitangaza Taifa.
"Naimani kubwa na Rais wetu pia nawaomba wadhamini nao wasiutupe mchezo wetu huu unapeperusha vyema bendera ya Tanzania kupitia sisi na hiyo Agosti 14 nitawahahakikishia Watanzania mimi ni nani,"
Kwa upande wake Mratibu wa matukio kuelekea pambano hilo Beautrice Said amesema katika pambano hilo kutakuwa na mapambano ya utangulizi nane ya utangulizi ambayo yatawakitanisha mabondia wa hapa Tanzania.
Baadhi ya mapambano hayo ni Seleman Kidunda ambaye ataumana na Shaban Kaoneka uzito kg 72, Issa Nampepecha na Khareed Manjee kg 61.
Pia katika pambano hilo kutakuwa na pambano lingine la Kimataifa ambalo litamkutanisha Tony Rashid atakayemualika Mkenya Gabriel Ochieng pambano la raundi 12 kutetea ubingwa wa ABU.
Mwakinyo amepambana mapambano 18 na kupoteza mawili huku mpinzani wake Kayembe amecheza mapambano 12 kashinda 9 na kutoka sare 3. 

aliongeza kwa kusema kuwa mapambano mengine yatawakutania bondia Juma Choki dhidi ya Emanuel Mwakyembe na Baina Mazola atamkabili Haidari Mchanjo mbali na mapambano hayo kutakuwa na mapambano kumi kabla ya mpambano mkubwa wa Mwakinyo




Saturday, January 25, 2020

SUPER D AMUANDAA SUNDAY KIWALE KWA USHINDI WA K,O JANUARY 31 TANGA ATAKAPOZIPIGA NA YOHANA MCHANJA

Na Mwandishi Wetu
KOCHA wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye kwa sasa anamnowa bondia Sunday Kiwale 'Moro Best' kwa ajili ya mpambano wake wa kugombania ubingwa wa Dunia na Yohana Mchanja mpambano utakaofanyika January 31 katika uwanja wa Mkwakwani Tanga


Akizungumza wakati wa mazoezi ya kumuandaa Kiwale amesema kuwa kiwale yupo fiti sana hivyo mashabiki waje kwa wingi wangalie mchezo wa masumbwi yaliyokwenda shule kwa kuwa Kiwale yupo vizuri kwa asilimia mia moja sina shaka nae

aliongeza kwa kusema kuwa ushindi wa Kiwale ni K,O tu kwani sisi tunaenda Tanga kama wageni hivyo tunamtaka Mchanja ajiandae kweli kweli kwani sisi tunakuja na moto wenye kazi kubwa sana  hivyo atutofanya ajizi katika mpambano huo wa ubingwa wa dania wa U.B.O lazima tutarudi n mkanda Dar es salaam kwa mazoezi tuliyofanya 

aliongeza  kuwa katika mpambano huo pia ataenda na bondia wake mwingine Hassani Mgaya atakaezipiga na Saidi Mundi mpambano wa raundi sita hivyo mashabiki wa tanga waje kuona timu ya Super D inafanya nini siku hiyo ya january 31 katika uwanja wa Mkwakwani

na bondia Sunday Kiwale amesema yeye kama bondia amejiandaa na yupo tayali kwa mchezo ata sasaivi kwani yupo fiti sana ata hivyo tuataanza safari ya kutoka dar siku ya alhamisi na tukifika siku hiyo tutamima uzito kwa ajili ya mpambano siku ya pili yake naomba wakazi wa tanga na vitongoja vyake waje kuangalia ngumi mawe masumbwi
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto akimfundisha bondia Sunday Kiwale 'Moro Best' jinsi ya kupiga ngumi ya mkunjo wa chini 'UPCAT' kwa ajili ya maandalizi ya mpambano wa bondia huyo utakaofanyika january 31 katika uwanja wa Mkwakwani Tanga ambapo atazipiga na Yohana Mchanja 

Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' akimwelekeza jinsi ya kupiga ngumi zilizo nyooka bondia Sundasy Kiwale 'Moro Best' ambaye anajiandaa na mpambano wake na Yohana Mchanja utakaofanyika January 31 katika uwanja wa mkwakwani Tanga



Friday, September 27, 2019

BONDIA MAKUBI ATAMBA KUMPIGA ABDALLAH MA MOROGORO OKTOBA 4 KATIKA UKUMBI WA 361 MWENGE

Na Mwandishi wetu 

Bondia Ibrahim Makubi yupo kambini kwa ajili ya mazoezi yake ya kumkabili bondia abdallah kingolwira  wa ( morogoro ) katika pambano lake litakalo fanyika Oktoba 4 katika ukumbi wa 361 uliopo mwenge jeshini mpambano huo ambao umewekwa kwa ajili ya kupandisha viwango mabondia mbalimbali litakuwa ni sehumu moja ya kuwapongeza mabondia

waliofanya vizuri nje ya nchi na kurudi na mikanda mikubwa nchini miongoni mwa mabingwa hao ni Abdalah Pazi ,Tonny Rashidi ,Bruno Vifua Viwili mabondia hawo wameleta mikanda hiyo nchini ndani ya mwezi mmoja tu

Makubi ametamba kumsambalatisha bila huruma yoyote ile Abdalah wa morogoro kwani ushindi wake ndio utakao msafishia njia ya kwenda juu zaidi katika mapambano ya ngumi anajua kuwa ngumi sio mchezo raisi kama ilivyo kwa michezo mingine

nae kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' anaemnowa na kumtafutia mambambano kwa ajili ya kumpandisha Daraja bondia huyo amesema kwa sasa makubi kila pambano lake kwake ni fainal kwani hapa kazi tu No Pain No Gain tutaakikisha tunashinda kila pambano na mpaka atakuwa bingwa wa mabingwa nchini na Duniani alisema Kocha  Super d

BONDIA JUMA CHOKI SASA AWAZIA UBINGWA WA TAIFA BAADA YA KUWA KING OF THE RING

NA MWANDISHI WETU

BONDIA Juma Choki Baada ya kumgalagaza bila ya huruma Emanuel Mwakyembe na kuchukua ubingwa wa King Of The Ring 2019 katika uzito wa KG 58 amesema ato bweteka kwa kuwachua ubingwa huo 

ambapo alipewa zawadi ya pikipiki pamoja na kitita cha shilingi laki tano amesisitiza ato bweteka kwa kuwa bingwa wa mashindano hayo ata hivyo ameomba kuwa andaliwe ubingwa wa taifa ndio matarajio yake kwa sasa akichukuwa ubingwa wa taifa kisha ataenda juu kuchukuwa ubingwa wa Afrika arafu ubingwa wa Dunia

Bondia huyo mwenye ndoto ya kuwa bingwa wa Dunia kupitia mchezo wa masumbwi nchini Tanzania kwa kuchukuwa mikanda nje ya nchi na kuletea sifa Tanzania 

Akizungumza kocha wake ambaye ni kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa choki ni bondia mzuri na malengo yake ni kufika mbali na kweli atafika anapo pataka kwani kwenye nia pana njia

ikumbukwe kuwa mimi ndio nimewatoa mabondia mabingwa wa dunia ambao wamepita katika mikono yangu kama vile Ibrahimu Class 'King Class Mawe' Idd Mkwela Vicent Mbilinyi Sunday Kiwale Ibrahimu makubi ambaye kwa sasa yupo mazoezini akijiandaa na mpambano wake na abdallah kingolwira wa morogoro pambano litakalofanyika Oktoba 4 katika ukumbi wa 361 mwenge pale jeshini

hivyo nina uwakika na mabondia wangu wote ninaowafundisha na siku zoto sinaga kazi mbovu


NGUMI KUPIGWA IJUMAA OKTOBA 4 UKUMBI 361 MWENGE

Mabondia wa mgumi za kulipwa nchini walioibuka na ushindi wanatarajia kushiriki katika sherehe za kupongezwa na mashabiki wao Oktoba Nne Club 361Mwenge Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Mwandishi wa Habari hizi Mratibu mkuu wa Pambano la kuwapongeza mabondia hao Selemani Semunyu alisema mipango imekamilika ikiwemo mabondia watakaocheza ingawa maombi ni mengi ya mabondia wengi kutaka kushiriki kuonyesha furaha yao na kuwaunga mkono mabondia wenzao .
Aliwataja miongoni mwa mabingwa hao ni Abdalah Pazi ,Tonny Rashidi ,Bruno Vifua Viwili na Nassib Ramadhani kwa pamoja na bondia yeyote bingwa na wameletea taifa heshima kubwa wadau na mashabiki hakuna budi kuwapongeza.

" Serikali na Wabunge wamewapongeza lakini wadau na mashabiki sasa huu ndio wasaa wa kuwapongeza hata kama kuna zawadi ya kuwapa hii ndio sehemu moja lakini sie tunawapongeza kwa pambano" Alisema Semunyu.
Aliongeza kuwa pambano hili pia litatumika kupata mabondia watakaowania mikanda mwezi Desemba ambapo litafanyika pambano la funga mwaka.
" Watakaofanya vizuri katika pambano hili wataweza kupata nafasi katika pambano la mwezi wa 12 ambapo historia ya Ngumi nchini kwa kipindi cha hivi karibuni itawekwa " Alisema Semunyu.
Pia amewashukuru kamisheni ya ngumi za kulipwa kutoa kibali kwa wadhamini Smart Gin na kuomba wadhamini wengine kujitokeza kwa wingi ili kufanikisha kurejesha hadhi ya mchezo wa ngumi nchini.
Kwa upande wake mratibu wa kiufundi wa mapambano hayo Yassin Abdalah Ustaadh aliwataja mabondia watakaosindikiza sherehe hiyo kuwa ni issa nampechehe (Dsm) vs alli hamisi (morogoro )
Ibrahim Makubi (Dsm)vs abdallah kingolwira ( morogoro )Maganga kulwa (mbagala) vs Said Sudi (M'nyamala) )Hashimu msungo vs Epson john Lewis Salumu omari vs ramadhani chicho
Aliongeza kuwa mapambano yanaweza kuongezeka kutokana na mabondia wengine kutafuta nafasi ya kutaka kushiriki Desemba lakini wengine nao wanataka kushiriki kuonesha furaha ya ushindi huo

Saturday, September 14, 2019

MABONDIA JUMA CHOKI NA EMANUEL MWAKYEMBE WAPIMA UZITO KUPIGANA KESHO SEPTEMBA 15 MASAKI

Bondia Juma Choki akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Emanuel Mwakyembe utakaofanyika katika ukumbi wa Backet Lounger Septemba 15 kushoto ni katibu wa Kamisheni ya ngumi Tanzania TPBRC Yahya Pori

Bondia Juma Choki akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na mpinzani wake Emanuel Mwakyembe kulia mpambano utakaofanyika katika ukumbi wa Backet Lounger Septemba 15 Jumapili 

Bondia Juma Choki na Emanuel Mwakyembe wakitunisha misuli mbelew ya kamera mabondia hawo wamepima uzito na Afya kwa ajili ya mpambano wao wa Septemba 15 katika ukumbi wa Bucket uliopo Masaki jumapili hii

Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila Super D kushoto akiwa katika picha ya pamoja na Jumachoka na kocha Edward Lwiyakwipya na bondia Emanuel Mwakyembe


NA Mwandishi wetu

MABONDIA Juma Choki na Emanuel Mwakyembe wamepima uzito kwa aqjili ya mpambano wao kwa ajili ya mpambano wa King Of The Ring utakaofanyika Septemba 15  katika ukumbi wa Backet Lounger uliopo Masaki Dar ES salaam

Mabondia hawo wamefanikiwa kufika Fainal baada ya kuwashinda wapinzani wao katika hatua za awali mshindi katika mpambano huo atanyakuwa pikipiki pamoja na kitita cha shilingi laki tano na atakaepigwa atachukuwa flat TV kubwa pamoja na kitita cha shilingi laki tano

Promota wa Mpambano huo Crisiani Kisinini amesema kuwa mbali na mpambano uho kutakuwa na mapambano mengine ambapo bondia Issa Nampepeche atazipiga na Emanuel Timtimu na mabondia wengine wengi


Aliongeza kwa kusema kuwa mapambano ya ngumi yataanza saa moja kamili usiku  uki kila likipigwa pambano moja kunakuwa na burudani na mpambano wa mwisho kabisa utafanyika saa tano na saa sita itakuwa mwisho na atajulikana nani ni champion wa mashindano ya King Of The Ring ambapo Mshindi wa kwanza mpaka wa tatu watajinyakulia zawadi kubwa

Mshindi wa kwanza ataondoka na Pikipiki pamoja na laki tano pesa taslim na wa pili atajinyakulia flat TV kubwa pamoja na Laki tano wa tatu atachukuwa kiasi cha pesa Taslim shiling Laki Tano

Hivyo amewataka wapenzi wa mchezo wa masumbwi waje waangalie nani bingwa katika uzito wa KG 58 kwa hapa nchini Tanzania



Tuesday, September 10, 2019

JUMA CHOKI AJIFUA KUMKABIRI MWAKYEMBE SEPTEMBA 15

Bondia Juma Choki kushoto akioneshana umwamba na bondia wa Kimataifa ambaye alishawai kuishi nchini Marekani miezi takribani 8 kwa ajili ya mchezo wa masumbwi nchini humu Ibrahimu Class 'KING CLASS MAWE' Choki anajiandaa na mpambano wake wa fainal dhidi ya Emanuel Mwakyembe septemba 15 katika ukumbi wa bucket club uliopo Masaki Dar es salaam

Bondia Juma Choki kushoto akioneshana umwamba na Ibrahimu Makubi wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kambi ya Super D Coach iliyopo kariakoo

Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kushoto akioneshana umwamba na Juma Choki wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kamba ya Super D coach Shule ya Uhuru Dar es salaam Jana


Bondia Alex Kachelewa kushoto akitupiana makonde na Juma Choki wakati wa mazoezi yaliyofanyika katika kambi ya Super D coach shule ya Uhuru 


Bondia wa Kimataifa nchini Tanzania ambaye alishawai kuka nchini Marekani kwa Takribani ya miezi nane kwa ajili ya mcheszo wa masumbwi Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kushoto' akioneshana umwamba na Juma Choki anayejiandaa na mpambano wake dhidi ya Emanuel Mwakyembe utakaofanyika septemba 15 katika ukumbi wa Backet club ulipo masaki


Bondia wa Kimataifa nchini Tanzania ambaye alishawai kuka nchini Marekani kwa Takribani ya miezi nane kwa ajili ya mcheszo wa masumbwi Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kushoto' akioneshana umwamba na Juma Choki anayejiandaa na mpambano wake dhidi ya Emanuel Mwakyembe utakaofanyika septemba 15 katika ukumbi wa Backet club ulipo masaki


Na Mwandishi Wetu

Bondia Juma Choki anaye jiandaa na mbambano wake dhidi ya Emanuela Mwakyembe septemba 15 katika ukumbi wa bucket Clab uliopo Masaki jijini Dar es es salaam amejinasibu kumtwanga bondia huyo na kuchukuwa ubingwa wa king of The Ring 

akijinasibu bondia huyo alivyotembelewa kambini kwake kwa Super D Coach iliyopo shule ya Uhuru Jijini Dar es salaam 

Amesema kuwa mwakembe ana uwezo wa kukanyaga moto wake ata siku moja huko alikutana na viande sasa kaja kwenye kazi kazi hapo  ndipo pa kuoneshana uwezo kama anavyosemaga kocha Super D Kazi Kazi No Pain No Gain yani siku hiyo patachimbika hivyo mwakyembe ajipange sana kwana mazoezi ninayofanya na mbinu ninazofundishwa sio za kitoto hatari tupu

Nae kocha wa bondia huyo Rajabu Mhamila 'Super D' amesema hii ni vita kubwa sana kwa kuwa kocha wa mwakyembe  Edward Lwiyakwipya wamesoma nae pamoja katika ngazi kubwa ya kozi ya kimataifa hata hivyo mimi nina mbinu nyingi zaidi yake ata hivyo nita akikisha napata ushindi usiokuwa wa kuwachosha majaji hivyo matumaini yangu ni kumpiga k,o mbaya zaidi

ikumbukwe kuwa mabondia wote wenye viwango vya juu nchini wanatoka kwangu ukiangalia mabondia wote wakubwa wanatoka kwangu na wana viwango vya kimataifa hivyo najivunia kwa hilo ukiangalia mabondia wanaotoka kwangu akuna ata mchovyu mmoja alijinasibu Super D

Aliongeza kwa kusema mikono yake wamepita mabondia wengi sana akiwemo Sanday Kiwale, Idd Mkwera Vicent Mbilinyi Ibrahimu Class' King Class Mawe' Shomali Milundi  Shabani Kaoneka na mabondia mbalimbali nchini wote wamepita katika mikono yangu kwa njia moja au nyingine hapa ndio No Pain No Gain kazi kazi hivyo wapenzi wa ngumi muje kwa wingi kuangalia kazi hii ambayo aita muacha mtu salama