Tangazo

Pages

Friday, June 3, 2016

Maskini Muhammad Ali! Alazwa tena hospitalini


https://i.ytimg.com/vi/C_fEIVwjrew/maxresdefault.jpg
Muhammad Ali katika moja ya mapambano yake akimuadhibu mpinzani wake aliyelala sakafuni.
UNAMKUMBUKA Bingwa wa Dunia wa Masumbwi uzani wa juu wa zamani Muhammad Ali? Ni hivi. Jamaa huyo aliyewatetemesha mabondia wenzake amelazwa hospitalini kufuatia maambikizi ya mapafu.
Bondia huyo nyota mwenye umri wa miaka 74 aliyekonga nyoyo za wapenzi wa ndondi kote duniani anasemekana kuwa katika hali wastani alipolazwa hospitalini.
Hata hivyo familia yake ilipendekeza alazwe hospitali kama tahadhari kwa sababu mbali na maambukizi hayo Ali anaugua kiharusi.
Bondia huyo alipatikana na ugonjwa wa Parkinson mwaka wa 1984 baada ya kustaafu mchezo huo wa ngumi za kulipwa.
Mara ya mwisho bondia huyo mkongwe alipolazwa hospitalini ilikuwa ni Januari mwaka uliopita baada ya kupatwa maambukizi ya njia ya mkojo.
Msemaji wa familia yake hata hivyo hakuwaambia wanahabari alikolazwa wala alilazwa lini.
Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment