Tangazo

Pages

Friday, September 28, 2012

CHEKA VS KALAMA WAPIMA UZITO LEO

Bondia Fransic Cheka akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake utakaofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba na Kalama Nyilawila siku ya jumamosi .Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Kalama Nyilawila akipima vipimo mbalimbali wakati wa kupima uzito leo
Bondia Kalama Nyilawila akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Fransic Cheka utakaofanyika siku ya jumamosi hii


KALAMA NYILAWILA FRANSIC CHEKA USO KWA USO JUMAMOSI HII


MIAMBA ya masumbwi nchini, bingwa wa Mabara Francis Cheka [SMG] na aliyekuwa bingwa wa Dunia Karama Nyilawila [Kapten] wanatarajia kupanda ulingoni Jumamosi mwaka huu kuoneshana umwamba.
Cheka na Nyilawila walitwangana mbambanmo wao uliofanyika morogoro ata hivyo ulizua utata baada ya mpambano wao kugubikwa na alama za mshangao ambalo cheka aliibuka na ushindi wa point  mashabiki kuhisika wa mabondia hao wanaogopana na kutafutana kwa mda mrefu watapoza kiu yao kwa mpambano huo jumamosi ya kesho.

Akizungumza Dar es Salaam jana, promota wa pambano hilo Oswald Mlay alisema pambano hilo litapigwa katika uwanja wa PTA Sabasaba
.
Alisema pambano hilo litakuwa la raundi 12 uzito wa kg 72 ambapo leo wamepima uzito kwa ajili ya mpambano uho utakaoamua nani zaidi

Katika Mchezo huo kutakua na Uhuzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha wa mchezo huo mkoa wa kimichezo wa Ilala Rajabu Mhamila 'Super D' kwa ajili ya kuwapa mambondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi.

Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi.




Super D Boxing Coach
Email.superdboxingcoach@gmail.com
www.burudan.blogspot.com
www.superdboxingcoach.blogspot.com
 Mob;+255787 406938
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

No comments:

Post a Comment