Tangazo

Pages

Tuesday, September 30, 2014

MPAMBANO WA NGUMI KUPIGWA SIKU YA NYERERE DAY TANDIKA

Na Mwandishi Wetu

BONDIA Imani Daudi anatarajia kupigan
a na Patrick  Amote kutoka kenya kwenye mpambano wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi utakaofanyika katika ukumbi wa musoma bar Tandika siku ya kumbukumbu ya baba wa Taifa Nyerere Day tarehe 14 mwezi huu mpambano huo unaoratibiwa na oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO chini ya Rais wake Yassin Abdallah 'Osthadhi'

lina marengo ya kumkumbuka baba wa taifa katika siku hiyo ya kipekee kabisa kwa nchi yetu ya Tanzania

akizungumza na mwandishi wa habari hizi Abdallah amesema kuwa kila mwaka wanafanya hivyo kwa ajili ya kumkumbuka baba wa taifa hili ambaye alipenda michezo mbalimbali bila ubaguzi wa aina yoyote hile ingawa kwa sasa michezo inabaguliwa kwa mingine kupewa ufadhili na mingine kupewa kidogo na mingine kunyimwa kabisa ufadhili

aliongeza kuwa siku hiyo pia kutakuwa na mipambano mbalimbali ya utangulizi moja likiwa bondia Shomari Milundi atamenyana na Suma Ninja na mapambano mengine mbalimbali

nae bondia Imani Daudi amejidhatiti kufanya kweli kwa kumsambalatisha Amote wa kenya ili aendeleze wimbi lake la ushindi na kuvutia mashabiki zaidi katika mchezo huo wa masumbwi

siku hiyo pia kutakuwa zikiuzwa DVD mpya za masumbwi ambazo zinaonesha mafunzo mbalimbali ya mchezo wa ngumi yanavyoanza hatua kwa hatua

mpaka kujua kitu kamili katika


mchezo huo pia kunakuwa na mapambano ya mabondia mabigwa wa dunia wa mchezo huo kama Floyd

Maywether, Manny Paquaio,mike Tyson, Mohamed Alli pamoja na mabambano ya ngumi ya ndani

No comments:

Post a Comment