Tangazo

Pages

Thursday, December 12, 2013

MATEKE KUPIGWA KATIKA PAMBANO LA JAPHET KASEBA DESEMBA 22



LILE pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa kati ya  bondia, Alibaba Ramadhan na bingwa, Japhet Kaseba, sasa litakuwa na sura mpya ya mapigano, baada ya muandaaji wa pambano hilo, Ibrahim Kamwe,  kuongeza mapambano  la  mchezo wa Kick Boxing (ngumi na mateke) ili kuleta radha zaidi.

Hatua hiyo imekuja baada ya bondia mtanzania anayeishi nchini Canada Kareem Kutch, ambaye anauraia wa nchini humo, aliyejigamba kuwa Tanzania hakuna wachezaji wa kiwango cha kimataifa wa mchezo huo na kutangaza kuwa hakuna  mtu wa kucheza naye hapa nchini,  jambo ambalo lilipingwa na mabondia wa mchezo huo, waliomtaka muandaaji wa pambano hilo, Bigright Promotion, afanye juhudi za kumleta nchini bondia huyo ili kujione vipaji.

Bigright, iliamua kumtafuta bondia `Tata Boy` ambaye amekubali kucheza na Mkanada huyo katika pambano la uzito wa Kg 75 za mchezo wa kimataifa.

Pambano hilo litakalopigwa siku ya jumapili ya Desemba 22, mwaka huu katika ukumbi wa friends corner hotel,  siku ambayo kutakuwepo na mapambano mengi yakiwemo ya Ernerst Bujiku, atakayezipiga na Sha Kasim, Lusekelo Daud, dhidi ya Mbaruku Heri, Issa Omar, atapigana na Haji Juma, Moro Best na Issa Peche na mapambano mengineyo mengi.

kwa ujumla ni mapambano ya kukaribisha sikukuu ya Krismas na mwaka mpya kwa staili ya aina yake na kuuaga mwaka kwa usalama na amani, ambayo yanasimamiwa na PST chini ya kiongozi wake Emanuel mlundwa.

No comments:

Post a Comment