Tangazo

Pages

Sunday, July 28, 2013

MADA MAUGO NA BENSON MWAKYEMBE WACHEZEA VICHAPO TOKA KWA WARUSSIA



MAUGO
BONDIA mada maugo  mwishoni mwa wiki iliyopita alichezea kichapo kutoka kwa  Movsur Yusupov wa Russia  katika mpambano uliopagwa kupigwa kwa raundi nane hata hivyo Maugo alipigwa kwa TKO ya raundi ya tano

ambapo Maugo alisalim amri kwa kupoteza mchezo huo ulifanyika katika viwanja vya Trade And Entertainment Centre "Moskva", Kaspiysk, Russia mwishoni mwa wiki iliyopita

Baada ya kupoteza mchezo uho August 30 atapanda tena uringoni kukabiliana na Thomasi Mashali mpambano wa ubingwa wa WBF Africa uzito wa kati mpambano utakaokuwa wa raundi 12
mwakyembe

Nae bondia benson mwakyembe alikuwa na kibarua kizito siku hiyo hiyo nae alikubali kichapo cha K,O ya raundi ya 7 katika mpambano wa raundi 8

Mabondia wote wawili walionesha kuwa na viwango vya kutosha ila walizidiwa ufundi na maarifa ya mchezo wa masumbwi uringoni
Mchezo wa masumbwi umekuwa ukipanda umaarufu siku adi siku baada ya mabondia wengi kutoka nje ya nchi kwenda kushiriki michezo mbalimbali katika nchi nyingine ambapo imeleta muhamko wa mchezo huo kupendwa na watu wengi zaidi ingawa wadhamini wanaukwepa kwa ajili ya kuwekeza katika mchezo huo

Hata hivyo kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini   Rajabu Mhamila 'Super D' amekuwa akitoa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi akitumia mabondia kutoka mataifa yanayofanya vizuri katika mchezo huo ili kujua mbinu mbalimbali wanazotumia

No comments:

Post a Comment