Tangazo

Pages

Saturday, July 20, 2013

Bondia Mbwana Matumla alilia mapromota wa masumbwi Tanzania



Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
BONDIA wa ngumi za kulipwa hapa nchini, Mbwana Matumla, amesema kwamba Tanzania bado inaandamwa na ukosefu wa mapromota, hali inayosababisha mchezo wa ngumi usifanye vizuri zaidi.
Bondia Mbwana Matumla, pichani.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Matumla alisema kuwa uhaba huo wa mapromota kunasababisha mabondia wengi washindwe kupata nafasi ya kuonyesha makali yao ulingoni.
Alisema endapo mapromota wangekuwa wengi, hata mwamko katika mchezo huo ungekuwa mkubwa, hivyo kuwafanya mabondia wapya kutamani zaidi tasnia hiyo ya masumbwi.

No comments:

Post a Comment