Tangazo

Pages

Saturday, February 8, 2014

SUPER D AJIVUNIA ZIARA YAKE YA MWAKA JANA


Na Mwandishi Wetu

Rajabu Mhamila Super D'
KOCHA wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila Super D' anajivunia mafanikio yake katika  mchezo
wa ngumi nchini baada ya mwanzoni mwa mwaka jana 2013 kufanya ziara ya mikoa 16 ya Tanzania bara

Aliyasema hayo wakati wa kufunga mashindano ya mchezo wa ngumi  yanayokwenda kwa jina la Nelson Mandela OpenChampion ship 'Unajua mimi mwaka jana nilifanya ziara ya kuamasisha mchezo wa masumbwi nchini nikiwa na lengo moja tu la ngumi zienee Tanzania nzima sasa naisi kazi niliyofanya imefanikiwa kutokana na mashindano haya kuja kushiliki watu wengi wa mikoani'

Super D ambaye katika kufuraishwa kwake kwa vijana wengi waliojitokeza mikoani kuja kushiliki alitoa DVD za Mafunzo ya mchezo wa masumbwi nchini kwa kila bondia aliyeshiliki kwa ajili ya kwenda kujifunza mbinu mbalimbali

pamoja na baadhi yao kuwapatia flana zenye nembo yake kama ishala ya kuhamasisha mchezo wa masumbwi ambazo amebuni mwenyewe zikiwa na mcholo wa  Glove pamoja na mahandishi yanayosomeka Super D Boxing Coach

aliongeza kwa kusema unajua mikoani kuna vipaji vingi sana hata hivyo bado awajawezeshwa kwa kuwa kwanza upatikanaji wa vifaa vya kufundishia ni tabu sana kwa watu wa mikoani hivyo wakiwezeshwa au wadau mbalimbali wakijitokeza kuwekeza kwenye mchezo huu unaweza ukapanda chati nchini
Super D ambaye anajishughulisha na uhuzaji wa vifaa vya mchezo huo amekuwa kiungo muhimu katika upatikanaji wa vifaa hivyo kwa mabondia na makocha kwa wepesi wa hali ya juu na kuufanya mchezo wa ngumi uzidi kusonga mbele kila kukicha nchini Tanzania


--
Super D Boxing Coach
Email.superdboxingcoach@gmail.com
www.burudan.blogspot.com
www.superdboxingcoach.blogspot.com
 Mob;+255787 406938
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

No comments:

Post a Comment