Tangazo

Pages

Tuesday, September 6, 2011

Changarawe aenda Uingereza na bondia mmoja kutoka mkoa wa ilala




MAKAMU wa Rais wa Shrikisho la Ngumi za Ridhaa (BFT), Michael Changarawe, ameondoka nchini na bondia mmoja kwenda kushiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola ya vijana walio chini ya umri wa miaka 18, yatakayoanza Septemba 8 hadi 13 mwaka huu nchini Uingereza.

Bondia wa Mkoa wa Ilala Mussa Mohamedi (kushoto) akioneshana ufundi wa kutupa masubwi na Salehe Omari wa Ngome wakati wa fainal ya michuano ya Klabu bingwa Dar es salaam . uzito wa kilo. 49 Light fly

Changalawe amesema ameondoka na bondia Musa Mohamed 'Dogo Musa', kwenda nchini Uingereza kushiriki michuano hiyo ya vijana itakayoshirikisha nchi mbalimbali.

Katibu wa shirikisho hilo, Makore Mashaga, amewapongeza mabondia walioshinda katika mapambano yao ya kwanza nchini Msumbiji katika michuano ya All Africa Games.

No comments:

Post a Comment