Tangazo

Pages

Thursday, August 4, 2011

WAZIRI WA HABARI ATEMBELEA MFUKO WA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA LEO





Mtendaji mkuu wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura (wa pili kutoka kulia) akiwatambulisha baadhi ya wafanyakazi wa mfuko huo kwa waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi (wa kwanza kulia) leo alipozitembelea ofisi za mfuko wa Vyombo vya Habari jijini Dar es salaam.
Mpiga picha kutoka Flame Tree Media Trust Bw. Mwanzo Millinga akimwonyesha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi baadhi ya picha za matukio mbalimbali alizopiga katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kutoa habari kwa umma kutokana na ufadhili wa Mfuko wa vyombo vya Habari (TMF) leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi( wa kwanza kulia) akiwa na Mtendaji mkuu wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura(kushoto) pamoja na wafanyakazi wa mfuko huo na waandishi wa habari wakiangalia moja ya kipindi cha Nchi Yetu kilichoandaliwa kwa ufadhili wa TMF kumulika Haki za Binadamu na masuala mbalimbali ya kijamii.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi (katikati) akitoa ufafanuzi wa baadhi ya picha zilizopigwa mkoani Lindi leo jijini Dar es salaam mara baada ya kutembelea Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi akiongea na wafanyakazi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) leo alipotembelea ofisi hizo kuona kazi mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo.Pamoja na mambo mengine kazi mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo.Pamoja na mambo mengine ametoa wito kwa mfuko huo kuhamasisha jamii kufanya kazi kwa bidii na kuibua masuala mbalimbali na fursa zilizopo nchini kwa maendeleo taifa.

EWURA Yapunguza Bei ya Mafuta


Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Haruna Masebu
Benjamin Sawe, Maelezo Dodoma

Serikali imepuguza bei ya mafuta ili kuwapunguzia makali watumiaji wa badhaa hiyo nchini.
Akizungumza na wanahabari Mkurugenzi wa EWURA Haruna Masebu amesema mafuta ya petroli yamepungua kwa sh 202.37 sawa na asilimia 9.17 ambapo mafuta ya dizeli yatakuwa yamepugua kwa shilingi 173 ambay ni sawa na asilimia 8.32.

Bwana Masebu alisema alisema bei ya mafuta ya taa imeshuka kwa shilingi 181.37 sawa na asilimia 8.70 na mabadiliko hayo yametokana na marekebisho ya yaliyofanywa na kanuni kukokotolea bei za mafuta.

Alisema bei zingeshuka kwa sababu ya kupanda kwa bei katika soko la dunia na kuendelea kushuka kwa tahamani ya shilingi ya Tanzania ikilinganishwa na dola ya Marekani.


Aidha Bwna Masebu alisema kwa mujibu ya Sheria ya mafuta ya mwaka 2008 bei za mafuta ya petrol I zitaendelea kupangwa na soko na EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta.

Alisema kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa za mafuta ya petrol kwa bei ya ushindani pasipo kuongeza bei iliyopangwa na taasisi ya EWURA.

Pia vituo vya mafuta vimetakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana ili kuonyesha bei ya mafuta.

Kwa mujibu wa Bwana Masebu bei hiyo ya mafuta itaanza rasmi kutumika rasmi

No comments:

Post a Comment