Tangazo

Pages

Tuesday, January 21, 2014

TUZO ZA PSPF BOXING AWARDS ZAZIDI KUHAMASISHWA

Bondia Antony Edowa kushoto akipambana na Gervas Regasiano wakati wa mchezo wao kwa ajili ya kuhamasisha tuzo za PSPF Tanzania Boxing Awards zilizofanyika nje ya uwanja wa karume karibu na soko la mitumba mchikichini Regasiano alishinda kwa point mchezo huo Picha na www.superdboxingcoac.blogspot.com

BAADHI YA VIONGOZI WA TUZO ZA PSPF TANZANIA BOXING AWARDS WAKIFATILIA MCHEZO WA WAZI ULIOFANYIKA NJE YA UWANJA WA KARUME KARIBU NA SOKO LA MITUMBA MCHIKICHINI KWA AJILI YA KUHAMASISHA TUZO HIZO ZINAZOFIKIA KILELE CHAKE JANUARY 25 KATIKA UKUMBI WA PTA SABASABA

Bondia Antony Edowa kushoto akipambana na Gervas Regasiano wakati wa mchezo wao kwa ajili ya kuhamasisha tuzo za PSPF Tanzania Boxing Awards zilizofanyika nje ya uwanja wa karume karibu na soko la mitumba mchikichini Regasiano alishinda kwa point mchezo huo Picha na www.superdboxingcoac.blogspot.com

Bondia Gervas Regasiano akinyooshwa mkono juu kuashilia ushindi wake baada ya kumtwanga Antony Edowa

Na Mwandishi Wetu

MCHEZO wa mwisho kwa ajili ya kuhamasisha ngumi unatarajia kufanyika siku ya alhamisi ya january 23 katika viwanja vya wazi vya Zakhem mbagala Dar es salaam mapambano hayo ya ngumi yenye lengo la kuhamasisha tuzo za PSPF Tanzania Boxing Awards ambazo zinafikia tamati january 25 kwa washindi kupatiwa tuzo hizo zitakazofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam

akizungumza na waandishi wa habari makamu wa rais wa shirikisho la ngumi za ridhaa nchini Lukelo-Willilo amesema utoaji wa tuzo hizo zitaongozwa na burudani mbali mbali na mapambano ya masumbwi ya mabondia wa ridhaa na kulipwa ambao wataoneshana uwezo siku hiyo alitaja burudani zitakazokuwepo siku hiyo kuwa na FM Academia, Malkia wa Mipasho Khadija Kopa, Excel one band,tom ongala, na kantona mgogo wa mazizi ndio burudani zitakazo tolewa kwa iku hiyo na mgeni rasmi

hatakuwa  Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fennela Mukangara ambaye atakukuwa akishudia kwa mara ya kwanza kabisa tuzo hizo  zinazoshirikisha mabondia mbalimbali 

na namna ya kupiga kula kuchagua bondia bora wa mwaka 2013,2014 unandia NGUMI (ACHA NAFASI)  andika namba ya mshiriki iliyoorodheshwa kwenye jina lake,kisha tuma kwenda namba 15573 kwa mfano ngumi 49 kwenda 15573 itakugalimu T.sh 150 kwa kila SMS  na unakumbushwa kupiga kula zaidi kadri 
uwezavyo kufanikisha  mwakilishi wako ananyakuwa tuzo hiyo 

No comments:

Post a Comment